Shirikisho la soka duniani Fifa limethibitisha kuwa katibu mkuu wake Fatma Samoura ameteuliwa kuwa 'Mjumbe mkuu wa Fifa kwa Afrika' katika jitihada ya kuimarisha utawala katika mchezo wa soka barani Afrika.
Shirikisho la soka barani Afrika (Caf) hivi karibuni limekuwa likichunguzwa katika masuala tofuati yanayohusisha uongozi na usimamazi.
Fatma, raia wa Senegal atachukua usukani kwa miezi sita kuanzia agosti mosi, huku wadhifa huo 'ukiwa na uwezo wa kuidhinishwa upya kwa makubaliano ya taasisi zote mbili'.
"Makubaliano yamefikiwa pia kwamba Fifa na Caf zitaidhinisha haraka iwezekanavyo uchunguzi wa ushahidi wa Caf," taarifa hiyo iliongeza.
Samoura, mwenye umri wa miaka 56, atasalia kuwa katibu mkuu wa Fifa lakini ataelekeza baadhiya majukumu kwa wengine katika shirikisho hilo.
Kwanini uamuzi huu, na una maana gani?
Fifa limeutaja uamuzi huu kama 'hatua ya kipekee na ya muda mfupi' wakai likibaini wazi majukumu atakayokuwa nayo afisa huyo wa zamani wa Umoja wa mataifa.
Wakati Fifa imezoea kuziteua kamati ambazo zinaendesha muungano wa waanchama yanayohitaji usaidizi, sio kawaida kwake kusaidia shirikisho zinazokuwa katika maatizo kama hayo.
Rais wa Caf Ahmad amekuwa akichunguzwa hivi karibuni katika nyanja mbalimbali, ikiwemo kuhojiwa na maafisa wa Ufaransa mjini Paris mapema mwezi huu kabla ya kuachiliwa huru pasi kushtakiwa.
Hili lilikuwa "sehemu ya uchunguzi kuhusu tuhuma za ufisadi, ukiukaji wa imani na udanganyifu" - huku kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 59 anayetoka Madasgascar akisema tuhuma zote zinazomuandama ni za uongo.
Masuala mengine ya hivi karibuni ni pamoja na mzozo kuhusu fainali ya ligi ya mabingwa Afrika na kupangwa upya muda wa fainali za mashindanoya kombe la mataifa bingwa Afrika 2019, 2021 na 2023.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
