Shirikisho la soka duniani Fifa limethibitisha kuwa katibu mkuu wake Fatma Samoura ameteuliwa kuwa 'Mjumbe mkuu wa Fifa kwa Afrika' katika jitihada ya kuimarisha utawala katika mchezo wa soka barani Afrika.
Shirikisho la soka barani Afrika (Caf) hivi karibuni limekuwa likichunguzwa katika masuala tofuati yanayohusisha uongozi na usimamazi.
Fatma, raia wa Senegal atachukua usukani kwa miezi sita kuanzia agosti mosi, huku wadhifa huo 'ukiwa na uwezo wa kuidhinishwa upya kwa makubaliano ya taasisi zote mbili'.
"Makubaliano yamefikiwa pia kwamba Fifa na Caf zitaidhinisha haraka iwezekanavyo uchunguzi wa ushahidi wa Caf," taarifa hiyo iliongeza.
Samoura, mwenye umri wa miaka 56, atasalia kuwa katibu mkuu wa Fifa lakini ataelekeza baadhiya majukumu kwa wengine katika shirikisho hilo.
Kwanini uamuzi huu, na una maana gani?
Fifa limeutaja uamuzi huu kama 'hatua ya kipekee na ya muda mfupi' wakai likibaini wazi majukumu atakayokuwa nayo afisa huyo wa zamani wa Umoja wa mataifa.
Wakati Fifa imezoea kuziteua kamati ambazo zinaendesha muungano wa waanchama yanayohitaji usaidizi, sio kawaida kwake kusaidia shirikisho zinazokuwa katika maatizo kama hayo.
Rais wa Caf Ahmad amekuwa akichunguzwa hivi karibuni katika nyanja mbalimbali, ikiwemo kuhojiwa na maafisa wa Ufaransa mjini Paris mapema mwezi huu kabla ya kuachiliwa huru pasi kushtakiwa.
Hili lilikuwa "sehemu ya uchunguzi kuhusu tuhuma za ufisadi, ukiukaji wa imani na udanganyifu" - huku kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 59 anayetoka Madasgascar akisema tuhuma zote zinazomuandama ni za uongo.
Masuala mengine ya hivi karibuni ni pamoja na mzozo kuhusu fainali ya ligi ya mabingwa Afrika na kupangwa upya muda wa fainali za mashindanoya kombe la mataifa bingwa Afrika 2019, 2021 na 2023.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
