Wednesday, May 15, 2019
Namna ya kuishi na ndugu wa mume
Ndoa nyingine zinaingia kwenye migogoro kutokana na kuingiliwa na ndugu wa mme pamoja na gubu za wanawake wa siku hizi, pamoja kwamba hawa wanawake wa siku hizi hawana uvumilivu na ni wakorofi haswa, lakini wakati mwingine ndugu wanaweza kuwa tatizo kwenye mahusiano yako wewe mwenza wako.
Wanaume wengi tumekuwa tukilichukulia hili suala kijuu juu lakini inawaumiza wenza wetu, jambo la kufanya kama mwanaume ijue tabia ya mkeo, na ndugu zako, kuna wanawake wanaficha makucha lakini hakikisha unaigundua, ili linapotokea tatizo iwe ni rahisi kufanya uchunguzi wako na kugundua nani mkorofi na ni nani ana matatizo.
Ishi mbali na ndugu zako kama mama unaweza kumjengea nyumba mbali na unapoishi ukawa unatuma mahitaji yote huko,utashangaa urafiki utakaokuwepo kati ya mkeo na mamako, hata akitaka kuja kukusalimia asikae muda mrefu sana mpaka kujenga mazoea.
Wakanye ndugu wengine wasiingie ndoa yako, kama kuna anachombeza vimaneno mpe onyo kali ambalo linamfanya aongoze, kitendo cha kuruhusu kuwasikiliza ndugu hupelekea kuletewa maneno ambayo huleta misukosuko kwenye ndoa.
Vilevile hata kama mke analeta maneno naye aonywe.Usiruhusu dada zako kuzoea kwako kama wameolewa wakae kwao watulie na familia zao hizi habari za kuja kuishi kwako mara kwa mara zinaweza sababisha migogoro kati yao na mke.
Kwa upande wa wanawake,mchukulie mama mkwe kama mzazi wako chochote atakachokutamkia kichukulie kawaida, lakini kabla ya kuolewa tambua kuna karaha kama hizo za ndugu wa mme na jua jinsi ya kukabiliana nazo.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
