MSANII wa Bongo Fleva, Abdulaziz Chende 'Dogo Janja' amefichua siri yake na msanii mwenzake, Faustina Charles 'Nandy' kwa kusema kuwa akiwa naye popote pale familia yake huwa na amani.
Dogo Janja aliyazungumza hayo leo katika mahojiano na kipindi cha Bongo 255 kinachoruka kupitia +255 GLOBAL RADIO ambapo alisema kuwa, alijuana na Nandy kabla hata hajaanza muziki.
"Nandy ni mshikaji wangu tangu zamani sana. Nakumbuka tangu hajaanza muziki wala kushiriki yale mashindano ya kuimba ambayo yalimtoa (Tekno Own Stage) yaliowahi kufanyika nchini Kenya na Nigeria.
"Ujue damu zetu zinaendana sana na ni mtu ambaye hata familia zetu zinafahamiana. Leo Nandy atakuja kwetu na mimi hivyohivyo kwao kwa hiyo hata nikiwa naye popote familia yake inakuwa na amani kabisa," alisema Dogo Janja.
Mbali na hilo, Dogo Janja pia alimuongelea msanii wa Bongo Fleva, William Lyimo 'Billnass' ambaye alidaiwa kutoka na Nandy kipindi cha nyuma kuwa akimuonea wivu atashangaa sana.
"Billnas hata akihisi kitu chochote kibaya kwangu mimi na Nandy atakuwa ni mtu wa ajabu sana. Ngoja nikwambie kitu, nikiwa na Nandy hakuna chochote kibaya kinaweza kutokea kati yetu," aliongeza Dogo Janja
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...