MAPOROMOKO ya udongo yaliyotokana na mvua kubwa yamesababisha vifo vya watu 60 katika mikoa ya Durban na KwaZulu-Natal nchini Afrika Kusini.
Zaidi ya watu 1,000 wameondoka kutoka makazi yao kwa mujibu wa Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ambaye ametembelea maeneo yaliyoathiriwa.
Mvua kubwa imekuwa ikinyesha katika maeneo ya kusini na mashariki mwa nchi hiyo siku chache zilizopita. Mafuriko zaidi na upepo mkali unatarajiwa katika maeneo ya pwani huku onyo likitolewa kuhusu hali mbaya ya hewa.
Mafuriko hayo makubwa yaliharibu biashara na nyumba za watu na vyuo vikuu viwili – huku mamia ya watu wakiondoka katika makazi yao.
Ramaphosa amezitembelea familia zilizopoteza wapendwa wao katika mafuriko hayo. Mwandishi wa BBC Nomsa Maseko amesema kuwa rais aliweka shada la maua katika eneo ambalo watu wanane walifariki.
Pia alionekana akiwasukuma walinzi waliokuwa wakiwazuia watu kusema naye.
"Ni muhimu kuja kuona kile kilichofanyika au kilichotokea na kuomboleza na familia zilizopoteza wapendwa wao katika janga hili. Kupoteza maisha sio jambo rahisi, hasa maafa yakitokea ghafla," alisema Ramaphosa.
Wakati hayo yakijiri, Waziri wa Tawala za Mikoa, Nomusa Dube-Ncube, amewaambia maofisa wa kituo cha radio cha SAFM kwamba bado wanaendelea kutathmini kiwango cha uharibifu uliosababishwa na mkasa huo, kwa mujibu wa shirika la habari la AFP.
Siku zijazo watu watalazimika kuhamishwa kutoka maeneo yaliyoathirika, alisema. Watu kadhaa wamepelekwa hospitali huku shughuli ya kuwatafuta manusura waliyozikwa chini ya vifusi vya majengo yalioporomoka.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...