Idara ya uhamiaji Mkoani Kagera imewakamata Tumaini Fransic na Peace Fransic raia wa nchi jirani ya Rwanda waliokuwa wanaishi hapa nchini kinyume cha sheria na kujifanya wWtanzania ambapo wameweza kupata elimu ya msingi, sekondari na chuo kikuu na kujipatia vyeti vya uraia kwa njia ya udanganyifu.
Mrakibu msaidizi wa Uhamiaji, Butenye Pendo amesema kuwa raia hao walizaliwa hapa nchini baada ya mzazi wao mmoja kuishi nchini kisheria ambaye ni mama yao mzazi lakini baada ya kumaliza elimu ya msingi na kujiunga na sekondari waliweza kutafta vyeti vya uraia ambapo mwenyekiti wa kijiji kyagati bw, Joseph Enerco Kanyonyi na wanawake walili Frida Samweli Kagemulo na Beatrice John Rweyemamu kujifanya wazazi wa watoto hao ili waweze kupata vitambulisho vya uraia na kuweza kupata mikopo ya elimu ya juu.
Afisa Pendo amesema kuwa Frida Samweli Kagemulo alisimama kama mama mzazi wa Tumaini Fransic na Beatrice John Rweyemamu kusimama kama mama mzazi wa Peace Fransic na mwenyekiti kuwasainia ili waweze kupata mikopo ya elimu ya juu kitendo ambacho kilifanikiwa huku wakijua kufanya hivyo ni kinyume na sheria.
Amesema kuwa sheria ya uraia namba 357 iliyofanyiwa marekebisho yake mwaka 2002 inaelezea aina za uraia ulipo hapa nchini kuwa ni; Uraia wa kurithi, Uraia wa kuzaliwa na uraia wa kuandikishwa ambapo mtu anaomba uraia wa kuishi hapa nchini kwa kufuata taratibu zilizowekwa kisheria.
Bw, Pendo amesema kuwa watuhumiwa watafikishwa mahakamani na kujibu tuhuma zinazowakabili huku akiwataka wananchi kuacha tabia za kuficha watu wasio wajua kwani wanaweza kujikuta wanakaribisha waharifu na majambazi ambao badae wanaweza kuvuruga amani waliyo nayo katika maeneo yao hasa watu wanaoishi mipakani.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...