Friday, March 29, 2019
Ukaribu wa Willy Paul na Nandy wahimarika, amwagia sifa
Baada ya mwimbaji Nandy 'African Princess' kufanya kolabo na Willy Paul kutokea +254 Kenya kwenye ngoma ya Njiwa ambayo iliachiwa rasmi June 27,2018 kaaika mtandao wa You Tube na kufanya vizuri ndani na nje ya nchi ya Tanzania, sasa wawili hao wanaonekana kuileta ngoma nyingine pamoja.
Kupitia ukurasa wa instagram wa Nandy ametuonyesha kipande kifupi cha video na kuandika caption ikisema 'Hallelujah" ambapo imetabiriwa kuwa ndio jina la ngoma inayofata na kisha akamtaja mwimbaji Willy Paul. Endapo ngoma hiyo ikitoka basi itakua ni track ya pili kutoka kwa mwimbaji Nandy na Willy Paul.
Inaelezwa kuwa ngoma hii inakuja baada ya kilio cha Willy Paul kutamani kufanya kazi tena na Nandy baada ya ngoma yao ya Njiwa kufanya vizuri huku akiwa ameshusha sifa kibao kwa mwanadada Nandy na kushukuru kwa kufanya nae project hiyo ya njiwa.
"Nandy ni mmoja wa wasanii wa kike wenye sauti Tanzania na Afrika kwa ujumla, ninafuraha kufanya nae kazi kwenye project ya njiwa, sitojali kufanya nae wimbo mwingine, kufuatia mafanikio ya njiwa sitojali kufanya nae nyingine tafadhali mwambieni sitojali kufanya nae nyingine, kama unatamani sisi kufanya wimbo mwingine basi andika neno ndio" >>>Willy Paul
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...