Wednesday, March 27, 2019
Mbao FC yaahidi kuifunga Simba tena katika ligi kuu
Kuelekea mchezo wa Ligi kuu Tanzania bara kati ya Simba SC na Mbao FC ya Jijini Mwanza utakaochezwa Machi 31 mwaka huu katika Uwanja wa Jamuhuri Mkoani Morogoro, Meneja wa Klabu ya Mbao FC Almas Moshi amesema kuwa wanauhakika wataifunga tena Simba SC katika mchezo huo.
Moshi amesema kutokana na Waalimu walionao kwa sasa ambao ni aliyekuwa Kocha mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania "Taifa stars" Salum Mayanga na msaidizi wake Novatus Fulgence,wanaamini watafanya vizuri katika mechi zao kutokana na uzoefu mkubwa walionao waalimu hao.
.
"Kutokana na waalimu tulionao kwa sasa tutafanya vizuri katika mchezo wetu na Simba japo Simba kwa sasa amekuwa akifanya vizuri katika Ligi kuu na mechi za kimataifa pia,lakini kwa uwezo walionao walimu wetu kwa mechi za kitaifa na kimataifa pia tutafanya vizuri na kuwafunga Simba tena" amesema Moshi
Klabu ya Simba SC sasa wanaotumia Uwanja huo Jamhuri kama Uwanja wao wa nyumbani baada ya Uwanja wa Taifa,Uhuru na Azam complex kufungwa ili kupisha maandalizi ya fainali za AFCON U17 ambapo Tanzania ndio mwenyeji.
Ikumbukwe kuwa Simba SC alifungwa bao 1-0 Septemba 20 mwaka jana na Mbao FC katika Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...