Wednesday, March 27, 2019
Mbao FC yaahidi kuifunga Simba tena katika ligi kuu
Kuelekea mchezo wa Ligi kuu Tanzania bara kati ya Simba SC na Mbao FC ya Jijini Mwanza utakaochezwa Machi 31 mwaka huu katika Uwanja wa Jamuhuri Mkoani Morogoro, Meneja wa Klabu ya Mbao FC Almas Moshi amesema kuwa wanauhakika wataifunga tena Simba SC katika mchezo huo.
Moshi amesema kutokana na Waalimu walionao kwa sasa ambao ni aliyekuwa Kocha mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania "Taifa stars" Salum Mayanga na msaidizi wake Novatus Fulgence,wanaamini watafanya vizuri katika mechi zao kutokana na uzoefu mkubwa walionao waalimu hao.
.
"Kutokana na waalimu tulionao kwa sasa tutafanya vizuri katika mchezo wetu na Simba japo Simba kwa sasa amekuwa akifanya vizuri katika Ligi kuu na mechi za kimataifa pia,lakini kwa uwezo walionao walimu wetu kwa mechi za kitaifa na kimataifa pia tutafanya vizuri na kuwafunga Simba tena" amesema Moshi
Klabu ya Simba SC sasa wanaotumia Uwanja huo Jamhuri kama Uwanja wao wa nyumbani baada ya Uwanja wa Taifa,Uhuru na Azam complex kufungwa ili kupisha maandalizi ya fainali za AFCON U17 ambapo Tanzania ndio mwenyeji.
Ikumbukwe kuwa Simba SC alifungwa bao 1-0 Septemba 20 mwaka jana na Mbao FC katika Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.
Source
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
