Sunday, February 24, 2019
Namna Sahihi ya Kupunguza Matumizi ya Mafuta ya Gari yako
Matumizi ya gari ni mojawapo ya matumizi makubwa kwa familia nyingi hasa zinazoishi mjini.
Inasemekana kwa wale wanaomiliki magari kuwa inawezekana nyumbani kukakosekana baadhi ya mahitaji mengine muhimu lakini gari ni lazima liwekwe mafuta na litembee. Je kuna ukweli wowote? Jaribu kufanya utafiti utaona. Watu wanalalamika uchumi mbaya lakini magari yanatembea.
Hii inamaanisha kuwa kwa maisha ya kisasa tunayoishi gari limekuwa mojawapo ya nyenzo muhimu na ya lazima. Lakini pia ni mojawapo ya kitu ambacho kinakula fedha nyingi toka mifukoni mwetu.
Kila mtu anatakiwa kutafuta jinsi ya kupunguza matumizi yanayotokana na gari. Mafuta ni sehemu mojawapo ya matumizi makubwa katika kumiliki na kuendesha gari.
Katika mada hii tunaangalia mbinu za kupunguza matumizi ya mafuta ya gari hivyo kuboresha uchumi wa wamiliki.
Mbinu za Uendeshaji Zinazosaidia Kupunguza Matumizi ya Mafuta ya Gari
Madereva wengi wanaendesha magari kwa namna ambayo inasababisha injini kula mafuta mengi sana. Kama utaendesha gari kwa kufuata mbinu hizi tu unaweza kupunguza matumizi yako ya mfuta kwa asilimia 10-20.
Zingatia Mwendo Kasi Sahihi
Kila gari linatumia mafuta katika namna tofauti, lakini katika spidi juu ya 90 Km/Saa mpaka 100 Km/Saa gari lolote huwa linatumia mafuta kidogo kuliko likiwa katika spidi nyingine. Kwa mjini huwezi kufikia spidi hii lakini jitahidi kuendesha juu ya 30 Km/Saa.
Pia fahamu kuwa spidi ikizidi 50Km/Saa mafuta yatatumika zaidi kwa kuwa gari linahitaji nguvu zaidi kushindana ukinzani wa hewa.
Zingatia: Zuia mwendo kasi kati ya 60-90 Km/Saa kwakuwa hutumia mafuta mengi
Usiongeze Mwendo Kwa Haraka
Kukanyaga mafuta kwa haraka ilikuongeza spidi kunachangia ulaji mkubwa wa mafuta. Unashauriwa kukanyaga mafuta taratibu unapoongeza mwendo kasi.
Unaweza ukasikiliza gari lako wakati unaendesha,ukisikia sauti kubwa unapoongeza mwendo ujue unachoma mafuta mengi na hivyo unaongeza gharama.
Usipunguze Mwendo Kwa Haraka- Acha Ukanyagaji Breki za Kushitukiza
Kama ilivyo katika kuongeza mwendo,unatakiwa kupunguza mwendo taratibu. Hakikisha kuna umbali wa kutosha kati yako na gari la mbele yako vinginevyo utajikuta ni lazima ukanyage breki kwa haraka na kwa kushitukiza ambako kunasababisha injini kula mafuta zaidi.
Kutobeba Mizigo Mizito Kwenye Gari
Uzito unapoongezeka katika gari hufanya injini kutumia nguvu nyingi kusukuma gari na hivyo kuhitaji mafuta mengi zaidi. Punguza mizigo isiyo ya lazima katika gari ukiwa unaendesha.
Kutoacha Gari Likiwa Linawaka Bila Kutembea
Utafiti unaonesha kuwa kwa wastani gari linatumia lita zipatazo 2 kwa saa kama likiwa linawaka bila kutembea. Sababu ni kuwa katika hali hii injini huwa inatembea na inahitaji mafuta kuzunguka.
Kama gari halitembei unashauriwa kuzima injini ili kupunguza matumizi ya mafuta.
Zingatia: Usiache gari likiwa linawaka zaidi ya dakika 1 bila kutembea
Zima Kiyoyozi (AC) Katika Mwendo Mdogo
Katika mwendo kasi wa chini ya 90 km/saa zima kiyoyozi na fungua madirisha. Kiyoyozi kinazungushwa na injini hivyo kutumia mafuta zaidi. Kukiwa unaenda spidi zaidi ya 90km/saa unatatumia mafuta kidogo ukifunga madirisha na kuwasha kiyoyozi.
Endesha Gari Likiwa na Matairi Yenye Upepo wa Kutosha
Matairi yenye upepo mdogo yanasababisha kuongezeka kwa eneo linalokanyaga barabara na hivyo nguvu nyingi inahitajika kusukuma gari.
Hakikisha matairi ya gari lako yana upepo katika viwango sahihi.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...