Sunday, December 2, 2018
Simba wakwea pipa Leo kuwafata Mbabane FC
Kikosi cha Simba ambacho kitacheza mchezo wa marudiano na timu ya Mbabane Swalows FC ya Eswatini kimepaa leo kuwafuata wapinzani wake kikiwa na tahadhari ya kulinda heshima ambayo walijiwekea katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Simba walifanikiwa kupata ushindi wa mabao 4-1 kwenye mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika, hivyo wanatakiwa wasifungwe zaidi ya mabao 2 watakapocheza Desemba 4 kwenye mchezo wa marudio ili kusonga mbele.
Ofisa habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa wanatambua wanakwenda kucheza na timu bora na kubwa, kazi yao ni moja kuweza kupata matokeo mazuri.
"Tunatambua tunakwenda kucheza na timu kubwa na bora, ila tuna kazi ya kulinda heshima yetu, tunajua sisi ni mabingwa wa Taifa na tunaliwakilisha, matokeo mabaya ni kujifedhehesha na kufuzu kwa Simba ni kujiweka sokoni kwa wachezaji kwenye rada za soka," alisema.
Safari yao ya leo watapitia Johannseburg, Afrika Kusini kisha watabadili ndege na kuelekea Manzini, Eswatini kwa ajili ya mchezo wao marudiano wa Ligi ya Mbaingwa Afrika dhidi ya Mbabane Swallows.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...