Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoani Tabora imewapandisha kizimbani Watumishi 7 wa halmashauri 3 za mkoa wa Tabora kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa.
Hayo yamesemwa na Kamanda wa taaasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoani Tabora, Mogasa Mogasa amesema kuwa katika kipindi cha Julai-Septemba 30 mwaka huu, jumla ya malalamiko 28 ya rushwa yalipokelewa na Taasisi hiyo na kufunguliwa mashtaka na sita kati yake yamefikishwa mahakamani.
Mogasa amewataja watuhumiwa wa shauri hilo la uhujumu uchumi kuwa ni Bikilile Mahyenga (Kaimu Mweka hazina) na Andrew Ndaba (Mhasibu) wanaokabiliwa na mashitaka mawili ya kughushi na kupokea rushwa.
Amesema kesi nyingine ni cc na.74/2018 dhidi ya Stephen Nyanda aliyekuwa Mhandisi wa halmashauri ya wilaya ya Uyui ambaye shauri lake lipo kwa Hakimu Mkazi Mfawidhi wa wilaya ya Tabora Sarafina Nsana na linatarajiwa kutajwa Novemba 28 mwaka huu.
Mogasa amemtaja mtuhumiwa mwingine aliyefikishwa mahakamani kuwa ni Emanuel Mwakasumule aliyekuwa Katibu wa Baraza la Ardhi kata ya Ziba wilaya ya Igunga ambaye anakabiliwa na kesi ya rushwa na. 1/2018.
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela amelishauri Kanisa la Kiinjili la Kilutheri ...
