Kampeni za uchaguzi wa urais zinaanza leo ya Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo huku kukiwa na mpasuko mkubwa kwenye upande wa upinzani na hofu juu ya usalama.
Mwisho wa wiki iliyopita wafuasi watatu wa chama tawala cha rais Joseph Kabila wanaripotiwa kuchinjwa katika jimbo la Kasai walipokuwa wakifanya kampeni.
Kura ya kumchagua mrithi wa Kabila aliyekaa madarakani kwa mika 17 itafanyika tarehe 23 ya mwezi ujao, Desemba 2018.
Wiki iliyopita Martin Fayulu alichaguliwa kusimama kama mgombea kinara wa upinzani na ameungwa mkono na wapinzani wengine wenye ufuasi mkubwa kama Moise Katumbi na Jean Pierre Bemba.
Hata hivyo, chama cha upinzani chenye wafuasi wengi zaidi nchini humo cha Union for Democracy and Social Progress tayari kimejitenga na mgombea huyo. Chama hicho kinaongozwa na Felix Tshisekedi kimekuwa mstari wa mbele dhidi ya utawala wa kabila.
Martin Fayulu (kati) alichaguliwa kusimama kama mgombea kinara wa upinzani lakini tayari wapo waliojitokeza kumpinga
Kiongozi mwingine wa upinzani Vital Kamerhe pia alijitoa kwenye makubaliano hayo akisema hakukuwa na uungwaji mkono wa kutosha kutoka mashinani baina ya wanachama.
Je Emmanuel Ramazani Shadary, ni nani?
Endapo mgogoro huo ndani ya upinzani utaendelea kupamba moto itakuwa ahueni kwa mgombea kutoka chama tawala Emmanuel Ramazani Shadary.
Shadary anaonekana na wengi kuwa ni kibaraka wa Kabila ambaye amezidisha muda wake madarakani kwa miaka miwili.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
