Tangu Rais wa Shirikisho la soka duniani (FIFA), Gianni Infantino aingie madarakani Februari 26, 2016, amekuwa akisisitiza zaidi mashirikisho ya soka katika nchi mbalimbali, kuhakikisha mpira wa miguu unachezwa kwa ngazi zote huku jukumu hilo likiwa chini ya Mkurugenzi wa ufundi.
Baada ya jana Oktoba 22, 2018 shirikisho la soka nchini TFF kumtangaza rasmi kocha Ammy Ninje kuwa mkurugenzi wake wa ufundi, pia limeainisha majukumu yake ambayo yanakwenda sambamba na malengo ya rais wa FIFA ya kuhakikisha mpira wa miguu unasambaa kote.
Kwa mujibu wa TFF majukumu maalum ya mkurugenzi ni kuongoza mpango wa maendeleo na dira ya shirikisho katika masuala ya ufundi pamoja na kuhakikisha anafanya tathmini ya ufundi katika ngazi mbalimbali za soka nchini ikiwemo ligi kuu na madaraja mengine.
Jukumu jingine ambalo ni sehemu ya mipango ya FIFA katika kuhakikisha soka linaendelea, ni mkurugenzi kuhakikisha elimu ya soka inatolewa kwa makocha kwa kuandaa na kusimamia kozi mbalimbali za ufundi.
Ili kwenda sambamba na mahitaji ya ufundi katika ligi, ni jukumu la Mkurugenzi kusimamia vilabu kuajiri makocha wenye sifa na taaluma inayoendana na daraja la timu anayofundisha, na hapa ndipo leseni za makocha zinahusika.
Kubwa zaidi katika yote ambacho ndio kimekuwa kilio cha Rais Infantino ni mkurugenzi kuhakikisha anaandaa mpango wa kukuza soka kwa wakati ujao kwa kuhakikisha soka la vijana linakuwa na kuendelea kwa manufaa ya baadaye.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
