Tangu Rais wa Shirikisho la soka duniani (FIFA), Gianni Infantino aingie madarakani Februari 26, 2016, amekuwa akisisitiza zaidi mashirikisho ya soka katika nchi mbalimbali, kuhakikisha mpira wa miguu unachezwa kwa ngazi zote huku jukumu hilo likiwa chini ya Mkurugenzi wa ufundi.
Baada ya jana Oktoba 22, 2018 shirikisho la soka nchini TFF kumtangaza rasmi kocha Ammy Ninje kuwa mkurugenzi wake wa ufundi, pia limeainisha majukumu yake ambayo yanakwenda sambamba na malengo ya rais wa FIFA ya kuhakikisha mpira wa miguu unasambaa kote.
Kwa mujibu wa TFF majukumu maalum ya mkurugenzi ni kuongoza mpango wa maendeleo na dira ya shirikisho katika masuala ya ufundi pamoja na kuhakikisha anafanya tathmini ya ufundi katika ngazi mbalimbali za soka nchini ikiwemo ligi kuu na madaraja mengine.
Jukumu jingine ambalo ni sehemu ya mipango ya FIFA katika kuhakikisha soka linaendelea, ni mkurugenzi kuhakikisha elimu ya soka inatolewa kwa makocha kwa kuandaa na kusimamia kozi mbalimbali za ufundi.
Ili kwenda sambamba na mahitaji ya ufundi katika ligi, ni jukumu la Mkurugenzi kusimamia vilabu kuajiri makocha wenye sifa na taaluma inayoendana na daraja la timu anayofundisha, na hapa ndipo leseni za makocha zinahusika.
Kubwa zaidi katika yote ambacho ndio kimekuwa kilio cha Rais Infantino ni mkurugenzi kuhakikisha anaandaa mpango wa kukuza soka kwa wakati ujao kwa kuhakikisha soka la vijana linakuwa na kuendelea kwa manufaa ya baadaye.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
