Tuesday, September 4, 2018
Faida za Utumiaji Samadi Mashambani
Samadi ni aina ya mbolea ambayo hutokana na vinyesi vya wanyama mbalimbali kama ng'ombe, kuku, mbuzi, kondoo na wengine. Hii ni miongoni mwa mbolea ambazo wakulima wengi wanaweza kumudu kirahisi.
Vilevile mbolea zingine ambazo wakulima wanaweza kuzipata kwa urahisi ni masalio ya mimea shambani (mabiwi). Mfano wa masalio hayo ni kama mabua ya mtama, mahindi na mimea ya jamii ya kunde au kitaalamu hujulikana kama (leguminas). Masalio haya yakishaoza hurutubisha udongo kwa kurejesha chumvichumvi za madini zilizokuwa zimechukuliwa na mimea wakati inastawi.
Hata hivyo mbolea yenye manufaa zaidi ni samadi, kwani wataalamu wanakadiria kuwa tani moja ya vinyesi vya fahali (madume ya ng'ombe) huwa na thamani karibu kilo 6.3 za chumvichumvi za nitrates; tani moja ya samadi ya vinyesi vya ng'ombe majike huwa na kilo 5.1 za chumvi za nitrates.
Mbolea zinazotokana na masalio ya mimea kwa mfano, mabua ya mahindi tani moja hutoa mbolea inayoweza kurejesha ardhini karibu kilo 4.0 za chumvi za nitrates.
Hivyo samadi yenye mchanganyiko wa vinyesi vya ng'ombe majike na madume wanaofugwa kwa pamoja (wanaolala katika zizi moja) huwa na thamani kubwa.
Ili upate kustawi na kutoa mavuno mengi na bora, mimea huhitaji chumvichumvi za madini ya nitrates, phosphate na potash pamoja na kiasi kidogo sana cha chumvi za nitrates, phosphate na potash pamoja na madini ya boron, copper, manganese, zinc na nyinginezo.
Kwa hiyo rutuba ya udongo huwa inategemea sana kiasi cha chumvichumvi zilizomo udongoni.
Ubora wa samadi hukadiriwa pia kwa kiasi cha chumvi za madini zinazopatikana mathalani ng'ombe 50 wanaweza kutoa karibu tani 600 za samadi kila mwaka. Kiasi hiki cha samadi kinaweza kurejesha ardhini karibu kilo 3048 za chumvichumvi za nitrates, kilo 544 za phosphate na kilo 2722 za Potash, pamoja na kiasi kidogo cha Boron, Copper, Manganese na Zinc.
Wakulima au wafugaji wengi hufuga ng'ombe hata zaidi ya 50, lakini kwa wastani wengi huwa na idadi hiyo kama ni wastani wa ng'ombe ambao kila mkulima anaweza kuwa nao.
Mbolea yenye kilo 3048 za nitrates, kilo 544 za phosphate na kilo 2722 za potash kwa uwiano huo haziwezi kutengenezwa kiwandani kwani itakuwa ghali sana kiasi kwamba hakuna mkulima anaweza kununua.
Samadi kiasi hicho italeta manufaa mengi kwani licha ya kuongeza rutuba ardhini vilevile itaubadili udongo uwe katika hali nzuri zaidi kwa kustawisha mimea.
Kadhalika samadi unaufanya udongo ushikamane kwa nguvu zaidi hata usiweze kupeperushwa na upepo au kumomonyolewa na maji ya mvua.
Manufaa mengine ya mbolea ya samadi ni kuwa inaufanya udongo kuwa katika hali nzuri ya kuweza kuyashikilia maji au unyevu kwa muda mrefu.
Minyoo waishio udongoni ambao husababisha kuwepo nafasi kwa ajili ya hewa kupenya kwa urahisi na vijidudu vya bakteria ambavyo huozesha mbolea na kubadili hewa kuwa katika hali ya chumvichumvi zinazotumiwa na mimea, hupata mazingira mazuri kwa maisha yao katika udongo uliotiwa samadi.
Wataalamu wanasema kuwa ubora wa samadi inategemea jinsi ilivyokuwa imetunzwa zizini au kibandani kwani chumvi nyingi hasa zile za nitrates huwa zinapotea kwa urahisi kwa maji ya mvua, kutokana na kitendo chake cha kuyeyuka mara tu zinapolowa maji.
Ili tuendelee kuwa na thamadi kubwa ni muhimu zizi liwe na paa lisilovuja kusudi maji ya mvua yasilowanishe, la sivyo ng'ombe wafugwe katika vibanda.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...