Msanii na mtayarishaji wa muziki wa bongo fleva, Akili The Brain amesema ukimya wake katika muziki ulitokana na yeye kuwaacha wasanii wenzake watangulie kutoa kazi zao pamoja na kusoma soko jinsi lilivyo kusudi aweze kuachia ngoma zake.
Akili The Brain amebainisha hayo alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha PLANET BONGO 'PB', inayorushwa na East Africa Radio, muda mchache alipomaliza kutambulisha wimbo wake mpya wa 'mashallah'.
"Kabla sijaachia ngoma yangu, nilifanya 'research' kidogo juu ya watu wanataka kitu gani kwa sasa, pamoja na namna muziki jinsi ulivyo kwa sasa. Naweza kubadilika kutokana na 'time' inavyokwenda kusudi niweze kuwapa kile wanachokihitaji watu", amesema Akili.
Pamoja na hayo, Akili ameendelea kwa kusema kuwa "nina 'plan' kubwa ninayotaka kuifanya lakini kwa sasa siwezi kuiweka wazi, kwasababu kuna baadhi ya mambo bado hayajakaa sawa ila Mungu akijalia kila kitu kitakuwa sawa tu".
Mbali na hilo, Akili The Brain ameweka wazi kuwa mara nyingi hupendelea kuwatumia waandishi kuandika mashairi ya ngoma zake, kwa lengo la kutaka kuwatendea haki mashabiki zake.
Akili The Brain ni miongoni mwa wasanii walioweza kuiteka jamii katika miaka ya 2006 kwa vibao vyake kama Bongo Bhangra, Nakupenda Regina na nyingine nyingi.
Source
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...