Msanii na mtayarishaji wa muziki wa bongo fleva, Akili The Brain amesema ukimya wake katika muziki ulitokana na yeye kuwaacha wasanii wenzake watangulie kutoa kazi zao pamoja na kusoma soko jinsi lilivyo kusudi aweze kuachia ngoma zake.
Akili The Brain amebainisha hayo alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha PLANET BONGO 'PB', inayorushwa na East Africa Radio, muda mchache alipomaliza kutambulisha wimbo wake mpya wa 'mashallah'.
"Kabla sijaachia ngoma yangu, nilifanya 'research' kidogo juu ya watu wanataka kitu gani kwa sasa, pamoja na namna muziki jinsi ulivyo kwa sasa. Naweza kubadilika kutokana na 'time' inavyokwenda kusudi niweze kuwapa kile wanachokihitaji watu", amesema Akili.
Pamoja na hayo, Akili ameendelea kwa kusema kuwa "nina 'plan' kubwa ninayotaka kuifanya lakini kwa sasa siwezi kuiweka wazi, kwasababu kuna baadhi ya mambo bado hayajakaa sawa ila Mungu akijalia kila kitu kitakuwa sawa tu".
Mbali na hilo, Akili The Brain ameweka wazi kuwa mara nyingi hupendelea kuwatumia waandishi kuandika mashairi ya ngoma zake, kwa lengo la kutaka kuwatendea haki mashabiki zake.
Akili The Brain ni miongoni mwa wasanii walioweza kuiteka jamii katika miaka ya 2006 kwa vibao vyake kama Bongo Bhangra, Nakupenda Regina na nyingine nyingi.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...