Baadhi ya wasanii na wadau mbalimbali katika tasnia ya filamu wameona kuwa jambo linaliendelea katika mitandao ya kijamii kuhusu kumsema Steve Nyerere ni jambo baya na linamkosesha amani yeye na familia yake. Lakini pia jambo hilo limemfanya Steve ukata tamaa na kupoteza tena ule moyo wa kujitolea kila linapotokea jambo, na ndipo walipoanza kufunguka na kuomba wamuache Steve kumuandama kwa tuhuma za kuwa anakula pesa za rambirambi kweny misiba. Faiza Ally anasema , wasanii wa bongo movies wameshndea kuelewa umuhimu wa steve na ndio maana tangu tuhuma hizi zianze wamekuwa kimya bila kuongea chochote.Lakini pia yeye anamini kuwa Steve ni mtu muhimu sana katikati yao anaewaunganisha kwa moyo wake tena bila kulipwa wala kuombwa. Faiza anasema kuwa watu wanasahau kuwa steve amewasaidia mambo mengi tofauti na misiba , amekuwa nao katika harusi, katikakazi na dili nyingi mbalimbali lakini leo hii wanasahau na kukaa wakicheka tu pale wanapoona msanii huyo anatuhumiwa vibaya. Faiza anawaomba wasanii wote kusimama na kuungana pamoja ili kumtetea na kukanusha tetesi zinamzomkabili Steve Nyerere ili kuendelea kuweka heshima yake. Na kwa upande wa Aunty Ezekiel, anasema kuwa wasanii wamechagua kuzikwa na steve nyerere, hivyo waache kumbeza steve nyerere. kila binadamu huwa anapewa karama yakekatika hii dunia, tivu hiyo ni karama yake.jamani tuacheni tumeamua wenyewe kuzikwa na tivu….I love you tivu akee. Kwa upande wa soudy brown anasema kuwa pamoja na kwamba hapo awali jambo hili la steve llikuwa likichukuliwa kama utani lakini ifike sehemu waavche kuendelea kufanya utani kwa sababu inamkatisha tamaa mhusika,kwa sababu katika familia yoyote kuna mtu mmoja huwa anatokea kwa ajili ya kuwaunganisha watu wote.
Source
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Mamlaka za China zipo mbioni kudhibiti ongezeko la harusi za kifahari amabazo zimekuwa zikishamiri katika miaka ya karibuni. Kwamujibu wa ma...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...