Sunday, August 5, 2018
Wanachama wa Upinzani wakamatwa na kupandishwa mahakamani
Wanachama kadhaa wa chama cha upinzani nchini Zimbabwe (MDC) wamefikishwa mahakamani jana Jumamosi wakikabiliwa na mashitaka ya kufanya vurugu baada ya uchaguzi wa Jumatatu.
Wanachama hao wanaodaiwa kufanya vurugu katika ofisi za chama tawala pamoja na kuchoma moto magari wamerejeshwa mahabusu hadi ombi lao la kupata dhamana litakaposikilizwa kesho Jumatatu. Kiasi watu sita walifariki dunia baada ya wanajeshi kuwafyatulia risasi waandamanaji hatua iliyokumbusha kumbukumbu ya vurugu baada ya uchaguzi wakati wa utawala wa Robert Mugabe.
Mnangagwa amekishutumu chama cha Movement for Democratic Change- MDC kwa kusababisha vurugu na kuahidi kuunda tume huru kuchunguza mauaji hayo. Tume ya uchaguzi ilimtangaza Mnangagwa kushinda uchaguzi kwa asilimia 50.8 ya kura dhidi ya mgombea wa MDC Nelson Chamisa aliyepata asilimia 44.3 ya kura.
Mnangagwa mshirika wazamani wa rais Robert Mugabe ametoa mwito wa mshikamano ikiwa ni baada ya mshindani wake katika kuwania urais Nelson Chamisa wa chama cha MDC kuyakataa matokeo akisisitiza alikuwa ndiye mshindi katika uchaguzi.
Wakili wa upande wa utetezi Denford Helimani amesema wanaume 16 pamoja na wanawake wanane wamekamatwa ikiwa ni hatua dhidi ya upinzani.
Mnangagwa amekuwa akisisitiza kuwa uchaguzi wa Jumatatu ulikuwa huru na haki na kuusifia uchaguzi kuwa ni mwanzo mpya mnamo wakati akichukua hatua kukomesha kutengwa kwa Zimbabwe na Jumuiya ya kimataifa.
Waangalizi wa kimataifa wameusifu uchaguzi huo kuwa umefanyika kwa amani ingawa waangalizi wa Umoja wa Ulaya wanasema Mnagagwa alitumia taasisi za serikali pamoja na vyombo vya habari kushinda uchaguzi kutokana na kampeni za uchaguzi huo kutofanyika katika mazingira sawa ya huru na haki.
Chamisa mchungaji na mwanasheria mwenye umri wa miaka 40 ametoa mwito kwa wafuasi wake kujiepusha na vurugu wakati akitarajia kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani.
Mnangagwa aliye na umri wa miaka 75 anasema Chamisa yuko huru kupinga matokeo hayo ya uchaguzi mahakamani ingawa hatua hiyo inaonekana kupewa nafasi kidogo kubadilisha matokeo.
Mshirika huyo wazamani wa Robert Mugabe alichaguliwa kuongoza chama cha ZANU-PF baada ya Mugabe kujizulu Novemba mwaka jana kufuatia shinikizo la jeshi baada ya kukaa madarakani miaka 37.
Makundi ya haki za binadamu yameonesha wasiwasi kuwa hatua ya polisi kutumia nguvu zaidi dhidi ya waandamanaji ni dalili ya jinsi anavyotarajia kutawala nchini humo.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Siku moja baada ya Israel kusema kuwa inazidisha uvamizi wake wa ardhini nchini Lebanon, Hezbollah inadai iliwafukuza wanajeshi wa Israel ...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...