Sunday, August 5, 2018
Sababu ya Bocco kukaa benchi mechi za Uturuki
NA ELBOGAST MYALUKO
Baada ya mshambuliaji wa Simba John Bocco kukosekana katika mechi mbili za kirafiki ilizocheza timu yake nchini Uturuki ilipoweka kambi, idara ya mawasiliano yaweka wazi kuwa nyota huyo anapewa muda wa kupona vizuri.
Bocco ambaye ni nahodha wa Simba, amekosa mechi mbili za kirafiki, ambazo ni dhidi ya Mouloudia Oudja ya Morocco iliyopigwa Agosti 1, 2018 na ile ya F.C.E Ksaifa ya Palestina iliyopigwa jana Agosti 4.
Taarifa kutoka idara ya mawasiliano ya klabu hiyo imeeleza kuwa Bocco ambaye aliumia kwenye mechi za mwisho wa ligi anaendelea na programu maalum ili zimsaidie kupona vizuri na kurejea akiwa kwenye ubora.
Katika mechi hizo mbili Simba ilitoka sare ya bao 1-1 na Mouolodia FC bao la Simba likifungwa na Adam Salamba kabla ya kushinda mabao 3-1 jana dhidi ya F.C.E Ksaifa, mabao ya Emanuel Okwi mawili na Meddie Kagere moja.
Aidha taarifa pia imeeleza kuwa timu hiyo inatarajiwa kuanza safari leo ya kurejea jijini Dar es Salaam tayari kwa mechi ya tamasha la Simba Day itakayopigwa Agosti 8 dhidi Asante Kotoko kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa takwimu rasmi, John Bocco ambaye leo anasherehekea siku yake ya kuzaliwa, ndiye mfungaji bora wa muda wote wa ligi kuu soka Tanzania bara akiwa amefunga mabao 97 ndani ya miaka kumi aliyocheza akiwa na klabu za Azam FC na Simba SC.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
