Sunday, August 5, 2018
Sababu ya Bocco kukaa benchi mechi za Uturuki
NA ELBOGAST MYALUKO
Baada ya mshambuliaji wa Simba John Bocco kukosekana katika mechi mbili za kirafiki ilizocheza timu yake nchini Uturuki ilipoweka kambi, idara ya mawasiliano yaweka wazi kuwa nyota huyo anapewa muda wa kupona vizuri.
Bocco ambaye ni nahodha wa Simba, amekosa mechi mbili za kirafiki, ambazo ni dhidi ya Mouloudia Oudja ya Morocco iliyopigwa Agosti 1, 2018 na ile ya F.C.E Ksaifa ya Palestina iliyopigwa jana Agosti 4.
Taarifa kutoka idara ya mawasiliano ya klabu hiyo imeeleza kuwa Bocco ambaye aliumia kwenye mechi za mwisho wa ligi anaendelea na programu maalum ili zimsaidie kupona vizuri na kurejea akiwa kwenye ubora.
Katika mechi hizo mbili Simba ilitoka sare ya bao 1-1 na Mouolodia FC bao la Simba likifungwa na Adam Salamba kabla ya kushinda mabao 3-1 jana dhidi ya F.C.E Ksaifa, mabao ya Emanuel Okwi mawili na Meddie Kagere moja.
Aidha taarifa pia imeeleza kuwa timu hiyo inatarajiwa kuanza safari leo ya kurejea jijini Dar es Salaam tayari kwa mechi ya tamasha la Simba Day itakayopigwa Agosti 8 dhidi Asante Kotoko kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa takwimu rasmi, John Bocco ambaye leo anasherehekea siku yake ya kuzaliwa, ndiye mfungaji bora wa muda wote wa ligi kuu soka Tanzania bara akiwa amefunga mabao 97 ndani ya miaka kumi aliyocheza akiwa na klabu za Azam FC na Simba SC.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Siku moja baada ya Israel kusema kuwa inazidisha uvamizi wake wa ardhini nchini Lebanon, Hezbollah inadai iliwafukuza wanajeshi wa Israel ...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...