Saturday, August 18, 2018
Sababu 5 Zinazokufanya Uoe Au Kuolewa Na Mtu Ambae Si Chaguo Sahihi Katika Maisha Yako
KUNA baadhi ya sababu zinazosababisha watu kuoana pasipo kufanya maamuzi sahihi. Wanandoa wengi huingia katika ndoa wakitegemea mambo mengi kubadilika, kitu ambacho ni makosa yanayosababisha ndoa nyingi kuvunjika.
Kabla ya kuoa/kuolewa unapaswa Ujitambue Kwanza na ujiulize maswali kadhaa, kwanza jiulize; (1) Je huu ni wakati sahihi? (2) Kwa nini mtu huyu? na (3) Unamuoa au kuolewa na mtu atakaye kuwa sambamba na malengo yako katika maisha yako yote?
Wakati kuna sababu kadhaa za kumuoa/kuolewa na mtu sahihi, pia upande mwingine kuna sababu kibao zinazopelekea watu kuoa watu wasio sahihi kwao. Kabla ya kusema "Ndiyo" zingatia sababu tano hapa chini zinazokufanya uoe au kuolewa na mtu ambaye si sahihi ambae baadae hupelekea kutengana na kupeana taraka.
(1) Tumekuwa katika mahusiano kwa muda mrefu. Kuwa katika mahusiano kwa kipindi kirefu sio sababu pekee ya kufanikiwa kumpata mwenye mafanikio katika maisha yako, unaweza ukawa umemvumilia kwa muda mrefu na sasa ukaamua tu kwasababu umekwisha zoea tabia yake na kufuata usemi wa "maji ukisha yavulia nguo sharti uyaoge".
(2) Msukumo wa Marafiki - Rafiki zangu wote wamekwisha OA/KUOLEWA....... itabidi na mimi nioe/niolewe. Kufuata mkumbo wa makundi katika jamii sii kitu kizuri, kwani ndoa siyokitu cha kubeep na kuacha. Jipange kwanza na muda ukifika basi itaingia katika ndoa yenye mpangilio mzuri wa maisha.
(3) Sidhani kama nitaweza. Usipo jiamini na kujipenda mwenyewe sidhani kama itakuwa rahisi kumpenda mtu mwingine unayetegemea kuwa nae maishani.
(4) Mategemeo ya kuboresha tabia ya mwenza wako. Tukisha oana nitambadilisha tabia. Cheti cha ndoa siyo leseni ya kumrazimisha mwenzi wako kubadilika kwa lazima. Jaribu kuwa na subira na kumtafuta mwenzi mnae endana nae kitabia.
(5) PESA - Anakazi nzuri naamini ataleta pesa au anatoka katika familia ya kitajiri. Kunaukweli mkubwa katika misemo ya wahenga yani "kama ukiowa kwaajili ya pesa, basi utazilipa" japokuwa kuwa na pesa sio vibaya, lakini hii haitazuia pia haizuii kuwa na muunganiko mbaya wa ndoa.
Wanandoa wengi huingia katika dimbwi hili ambapo wengine hushinikizwa kuoa kulingana na taratibu za kimila au kidini. Lakini pia wazazi wakati mwingine huchangia ndoa nyingi kuvunjika, ikiwa ni kwa kuwachagulia wananandoa mke au mume.
Vijana ambao bado hamjaoa au kuolewa "Jitambueni Kwanza", fikirini kwa kina kabla ya kufanya maamuzi yasiyo sahihi ambayo yatawagharimu muda wenu na kupata mateso ya muda mrefu.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
