Saturday, August 18, 2018
Sababu 5 Zinazokufanya Uoe Au Kuolewa Na Mtu Ambae Si Chaguo Sahihi Katika Maisha Yako
KUNA baadhi ya sababu zinazosababisha watu kuoana pasipo kufanya maamuzi sahihi. Wanandoa wengi huingia katika ndoa wakitegemea mambo mengi kubadilika, kitu ambacho ni makosa yanayosababisha ndoa nyingi kuvunjika.
Kabla ya kuoa/kuolewa unapaswa Ujitambue Kwanza na ujiulize maswali kadhaa, kwanza jiulize; (1) Je huu ni wakati sahihi? (2) Kwa nini mtu huyu? na (3) Unamuoa au kuolewa na mtu atakaye kuwa sambamba na malengo yako katika maisha yako yote?
Wakati kuna sababu kadhaa za kumuoa/kuolewa na mtu sahihi, pia upande mwingine kuna sababu kibao zinazopelekea watu kuoa watu wasio sahihi kwao. Kabla ya kusema "Ndiyo" zingatia sababu tano hapa chini zinazokufanya uoe au kuolewa na mtu ambaye si sahihi ambae baadae hupelekea kutengana na kupeana taraka.
(1) Tumekuwa katika mahusiano kwa muda mrefu. Kuwa katika mahusiano kwa kipindi kirefu sio sababu pekee ya kufanikiwa kumpata mwenye mafanikio katika maisha yako, unaweza ukawa umemvumilia kwa muda mrefu na sasa ukaamua tu kwasababu umekwisha zoea tabia yake na kufuata usemi wa "maji ukisha yavulia nguo sharti uyaoge".
(2) Msukumo wa Marafiki - Rafiki zangu wote wamekwisha OA/KUOLEWA....... itabidi na mimi nioe/niolewe. Kufuata mkumbo wa makundi katika jamii sii kitu kizuri, kwani ndoa siyokitu cha kubeep na kuacha. Jipange kwanza na muda ukifika basi itaingia katika ndoa yenye mpangilio mzuri wa maisha.
(3) Sidhani kama nitaweza. Usipo jiamini na kujipenda mwenyewe sidhani kama itakuwa rahisi kumpenda mtu mwingine unayetegemea kuwa nae maishani.
(4) Mategemeo ya kuboresha tabia ya mwenza wako. Tukisha oana nitambadilisha tabia. Cheti cha ndoa siyo leseni ya kumrazimisha mwenzi wako kubadilika kwa lazima. Jaribu kuwa na subira na kumtafuta mwenzi mnae endana nae kitabia.
(5) PESA - Anakazi nzuri naamini ataleta pesa au anatoka katika familia ya kitajiri. Kunaukweli mkubwa katika misemo ya wahenga yani "kama ukiowa kwaajili ya pesa, basi utazilipa" japokuwa kuwa na pesa sio vibaya, lakini hii haitazuia pia haizuii kuwa na muunganiko mbaya wa ndoa.
Wanandoa wengi huingia katika dimbwi hili ambapo wengine hushinikizwa kuoa kulingana na taratibu za kimila au kidini. Lakini pia wazazi wakati mwingine huchangia ndoa nyingi kuvunjika, ikiwa ni kwa kuwachagulia wananandoa mke au mume.
Vijana ambao bado hamjaoa au kuolewa "Jitambueni Kwanza", fikirini kwa kina kabla ya kufanya maamuzi yasiyo sahihi ambayo yatawagharimu muda wenu na kupata mateso ya muda mrefu.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Mamlaka za China zipo mbioni kudhibiti ongezeko la harusi za kifahari amabazo zimekuwa zikishamiri katika miaka ya karibuni. Kwamujibu wa ma...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...