Monday, August 13, 2018

Mimi ni Legend Kwenye Bongo fleva- Dully Sykes

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Dully Sykes amefunguka na kuweka wazi kuwa katika muziki wa Bongo fleva yeye ndio Legend. Dully Sykes ameshawahi kutengeneza nyimbo kali kama Salome, Julietha, Hi na nyinginezo nyingi ambazo zilimpa umaarufu mkubwa sana kuanzia miaka ya 90 mpaka leo hii. Kwa ajili ya uwezo wake wa kukaa kwenye gemu kwa karibia miaka 20 sasa, Dully amekuwa akiwnda kwa jina la Legendari katika muziki huu wa Bongo fleva. Kwenye mahojiano na Sam Misago Tv, Dully amesisitiza kuwa yeye kweli ni legendary Kwenye muziki wa Bongo fleva ingawa Kwenye aina nyingine ya muziki kutakuwa na malegendari wengine: Nisipoitwa mimi legend ataitwa legend nani? Tukija Kwenye muziki wa Bongo fleva mimi ndio legend lakini Kwenye Muziki wa dansi Gurumo na Bi. Chuka na wengine ndio malegend". Dully ni msanii mkongwe ambaye ameweza kukaa Kwenye gemu kwa zaidi ya miaka ishirini huku akiwa hapotei kabisa kwani amekuwa na uwezo wa kutoa nyimbo na kuhit kwa miaka kadhaa.

The post Mimi ni Legend Kwenye Bongo fleva- Dully Sykes appeared first on Ghafla!Tanzania.


Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...