Monday, August 6, 2018

Masanja Amkingia Kifua Diamond platinumz, Asema Kuvaa Kikuku ni Sawa.

Mchungaji maarufu nchini masanja mkndamiza amefunguka na kumkingia diamond kifua huku akisema kuwa kwa mtu kuvaa kikuku ni kawaida tu kamawatu wengine wanapoamua kuvaa cheni hizo mikononi au shingoni au sehemu yoyote.

 Masanja anasema kuwa watu wamekuwa wanashindwa kutofautisha kati ya vitu hivi viwili kati ya dhambi na swala la maadili, kuna utofauti mkubwa kati ya dhambi na kile wasichokipenda watu kifanyike hivyo kwake kama mchungaji kuvaa kikuku sio dhambi.

"kama mchungaji kuvaa kikuku sio dhambi ,lakini unaambiwa kuwa katika maadili ni dhambi, na je nikawauliza kwani maadili ni nini.kwaio shida ipo katika maadili na hapo ndipo tunasema kuwa watu wanadhani kuwa  ni vile vitu wasivyovipenda wao.vitu visivyo na maadili mazuri wanadhani kuwa ni dhambi.kuna tofauti sana juu ya hivyo vitu viwili. narudia tena kuvaa kikuku sio dhambi kabisa."
The post Masanja Amkingia Kifua Diamond platinumz, Asema Kuvaa Kikuku ni Sawa. appeared first on Ghafla!Tanzania.

Source

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...