Sunday, August 12, 2018
Bocco kuikosa Mtibwa Ngao ya Jamii Jumamosi
Wakati kikosi cha Simba kikiwa katika maandalizi ya kujiwinda na mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya Mtibwa FC, kuna uwezekano mkubwa ikamkosa Nahodha wake, John Bocco.
Simba itashuka dimbani kukipiga na wakata miwa hao wa Morogoro katika mchezo wa Ngao hiyo Agosti 18 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Kuelekea mechi hiyo imeelezwa kuwa Bocco hajapewa nafasi kubwa ya kucheza kutokana na kutokuwa fiti kiafya kwa ajili ya kucheza.
Ikumbukwe Bocco aliukosa mchezo wa kirafiki dhidi ya Asante Kotoko Agosti 8 katika tamasha la Simba Day ambalo lilimalizika kwa sare ya bao 1-1 pamoja na jana dhidi ya Namungo FC huko Ruangwa, Lindi.
Aidha, taarifa za ndani zinasema Bocco anaweza akawakosa pia Tanzania Prisons, mechi ambayo itakuwa ni ya ufunguzi wa pazia la msimu mpya wa Ligi Kuu Bara utakaopigwa Agosti 22 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
