MWANAMKE mkazi Njage wilayani Kilombero Mkoa wa Morogoro, ameuawa kwa kukatwa kwa shoka kichwani na mumewe kwa kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi.
Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Willibrod Mutafungwa, alisema hayo jana na kufafanua kuwa tukio hilo lilitokea Julai 28 majira ya asubuhi ambapo mwanamke huyo, Rose Mngwe (43), aliuawa na mumewe, Jacob Kambo (45), mkazi wa Kijiji cha Njage.
Kwa mujibu wa Kamanda Mutafungwa, mwanaume huyo baada ya kumuua mkewe kwa kumkata kwa shoka kichwani, alikimbilia porini na kujinyonga kwenye mti kwa kutumia kamba.
Kamanda Mutafungwa alisema inadaiwa kuwa mwanaume huyo aliamua kufanya kitendo hicho baada ya kuona mkewe amempuuza alipomwambia kuwaondoa watoto wake wa kike aliowazaa nje ya ndoa.
Kamanda alifafanua kuwa alitaka waende kwa waliomzalisha watoto hao kwa madai kuwa wanawanyima nafasi wakiwa hapo.
Alisema miili ya marehemu hao imeshakabidhiwa kwa ndugu zao kwa ajili ya kuendelea na shughuli za mazishi.
Katika tukio lingine, Leo Charles Mashaka (61), mkazi wa Kitongoji cha Igagafu wilayani Kilosa, ameuawa kwa kupigwa na kitu chenye butu kichwani na usoni na mtoto wake wa kumzaa, Emmanuel Leo Charles, sababu ikitajwa ni kudai urithi.
Kamanda Mutafungwa alisema tukio hilo lilitokea Julai 30, alfajiri katika Kata ya Lumuma Tarafa ya Idete ambapo Mashaka alimpigwa na kitu chenye butu kichwani na usoni upande wa kulia na kumsababishia jeraha na michubuko mgongoni, Alisema tukio hilo lilisababishwa na mgogoro katika familia kuhusu urithi.
Kamanda huyo alisema mtuhumiwa alikamatwa na atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...