Jeshi la Polisi mkoani Mbeya linawashikilia watu wawili Judith Amoni Mwansansu(39) ambaye ni bibi wa mtoto na Aive Alex Swalo(17) shangazi yake, kwa kosa la kumfanyia vitendo vya ukatili mtoto, Daines Kefas Mwansasu(06) vya kumuunguza kwa moto na kumpiga.
Kamanda wa Polisi jijini humo, SACP Ulrich Matei, amesema tukio hilo lilifanyika Jumanne July 31, 2018 majira ya saa tatu usiku ambapo siku iliyofuata Jeshi la Polisi lilipokea taarifa za tukio hilo kutoka kwa raia wema kwamba mtoto huyo amejeruhiwa sehemu mbalimbali kwa moto.
"Inadaiwa siku hiyo ya Jumanne, Daines alikuwa ameenda kucheza na rafiki zake na aliporudi nyumbani majira ya jioni shangazi yake alimuadhibu kwa kumchapa na waya wa umeme sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia majeraha na maumivu makali mwilini", amesema Kamanda Matei.
Kamanda Matei ameongeza kuwa August 1, 2018 majira ya asubuhi, watuhumiwa (Shangazi akishirikiana na bibi wa mtoto) waliendelea kumfanyia vitendo vya ukatili mtoto huyo kwa kumuunguza kwa moto sehemu za miguuni na kwenye makalio.
Juni 16, 2018 katika kilele cha siku ya Mtoto wa Afrika, ambayo kitaifa ilifanyika mkoani Arusha na Tanzania ikitajwa kuongoza katika vitendo vya ukatili dhidi ya watoto kuliko uovu unaofanywa kwenye ujambazi, takwimu zilizowasilishwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto , Dk. Faustine Ndugulile, zinaeleza kuwa watoto 41,000 walifanyiwa ukatili kati yao 3,467 kwa kipindi cha Januari hadi Desemba mwaka jana.
Lakini pia, Idara ya Ustawi wa Jamii wizarani hapo, ilieleza kuwa asilimia 60 ya ukatili dhidi ya watoto unafanyika nyumbani, asilimia 53 ni shuleni na iliyobaki ni maeneo mengine.
Takwimu zinaonesha watanzania wengi hawajaweza kumlinda mtoto kwa mujibu wa sheria ya mtoto ya mwaka 2009, ambayo imetoa wajibu kwa kila mtu na adhabu kwa anayeshindwa kutekeleza jukumu hilo.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mjasiriamali Faiza Ally ameweka wazi hisia zake na kusema kuwa anatamani sana kuona msanii wa Bongo Flev...
-
UNAPOTAJA jina la mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' kutoka Tanzania, akili za wengi zinakimbilia kwe...
-
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya siku tano ya kunyesha mvua kubwa inayoweza kusababisha athari ikiwemo mafuriko. ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Geneva, Switzerland /AFP /.More than 100 groups urged the International Labour Organization to stop taking money from tobacco companies as t...