Thursday, September 12, 2024
Watu 800 Wavamia Kituo Cha Polisi Geita, Wawili Wauawa Kisa Kuhusu Watekaji wa Watoto
Wednesday, September 11, 2024
Oscar Oscar Amchana Mzize :Mchezaji wa Kawaida Sana Hajawai Ibabe Timu
KUHUSU ubora wa mshambuliaji wa Yanga na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Clement Mzize umekuwa na dosari kwa upande wa mchambuzi wa michezo Oscar Oscar ambaye alisema kwamba, mchezaji huyo licha ya kufunga mabao lakini hajawahi kufunga mabao ya kuibeba timu.
"Huu ni msimu wa tatu tunamshuhudia Mzize. Ni mchezaji mzuri sana, lakini hajawahi kufunga hata mabao 10 ya ligi. Hajawahi kufunga mabao ya kuibeba timu kwenye mazingira magumu na hana mabao mengi yanayokumbukwa na wengi.
"Natamani tungeacha mchezo wa kuongeza sifuri. Natamani tungeacha mchezo wa Waingereza. Mzize bado ni mchezaji ambaye kwenye nafasi tano anaweza kufunga bao moja. Bado anakua."
"Kuna watu wameanza kumpa jina na la Didier Drogba. Ni vizuri mtu kuwa na ndoto kubwa, lakini ni vizuri zaidi kuwa na ndoto zenye uhalisia. Tuna kijana anaitwa Kelvin John. Ni Mtanzania mwenzetu. Ni kijana wetu na anacheza Ligi Kuu Denmark. Wakati anaanza kuchipukia alipewa jina la Mbappe. Hadi leo hakuna mfanano wowote." Oscar Oscar
Tuesday, September 10, 2024
Mbozi wajipanga kukomesha ukatili kwa watoto
Na Baraka Messa, Mbozi
KUTOKANA na vitendo vya ukatili kukithir katika wilaya ya Mbozi mkoani Songwe Baraza la Madiwani Halmashauri hiyo limejipanga kupambana na janga hilo la ukatili vikiwemo vitendo vya ulawiti na ubakaji kwa watoto wadogo chini ya miaka nane.
Hayo yamebainishwa na katibu tawala wa Wilaya hiyo Mbwana Kambangwa akiongea na Habari Leo baada kikao cha baraza kamili la Madiwani kwa robo muhura mwaka 2023/2024 kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri hiyo ambapo amewataka madiwani kuongeza nguvu kwenye mapambano dhidi ya vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia katika maeneo yao.
"Matukio mengi ya ukatili kwa watoto wadogo yamekuwa yakiripotiwa na kuibuliwa na vyombo vya Habari mara kwa mara katika wilaya yetu ya Mbozi, hali hii imekuwa tishio kwa ustawi wa kizazi kijacho"
Amewataka madiwani ambao ni wawakilishi wa wananchi kujikita katika utoaji elimu mara kwa mara kuhusu madhara ya ukatili kwa watoto wadogo, ikiwa ni pamoja na kuwa karibu na watoto ili kubaini changamoto zinazowakabili ili wasaidiwe.
Kambangwa amesema pia wamepokea maelekezo kutoka Kwa Waziri Mkuu walipofanya kikao kupitia Mtandao ambapo kunamaagizo maalumu 13 walipewa ikiwemo la kupambana na ukatili wa Kijinsia huku akisema kuwa Mbozi ni miongoni mwa Wilaya zilizo kithiri kuwa na vitendo vya Ukatili wa kijinsia.
Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo George Msyani amesema Halmashauri inaendelea kupambana dhidi ya matendo ya kikatili huku mipango ikiwa juu ya kuendelea kutoa elimu Kwa jamii juu ya matendo ya Ukatili na kueleza athari zake.
" Tumepeana maagizo madiwani wote , suala la elimu ya ukatili katika kata zetu liwe ni ajenda ya kudumu, Kila diwani anapofanya mikutano atoe elimu kuhusu madhara ya ukatili kwa watoto wadogo tukishirikiane na watalaam wa ustawi wa jamii, maendeleo ya jamii pamoja na jeshi la polisi" alisema Msyani.
Kwa upande wake Neema Kibona alisema matendo ya Ukatili hasa Kwa Watoto wadogo yanazidi kushamili kutokana na uwepo wa kufichiana maovu kwa wanajamii hasa kwa kutaka kumaliza mambo kienyeji bila kufuata Sheria hali ambayo inaendelea kuwa changamoto kubwa.
Afisa elimu shule za msingi na awali wilaya ya Mbozi Dorothy Mwandila anasema ubize wa wazazi katika shughuli za kiuchumi kumekuwa na athari kubwa katika malezi ya watoto, kwani watoto wengi hulazimika kulelewa na watu wengine ambao sio wazazi na kupata madhara.
"Watoto wetu tuwalee wenyewe, tuache kuwategemea ndugu wengine na majirani kutulelea watoto wetu, kwa sababu matukio yaliyo mengi ya ulawiti na ubakaji kwa watoto chini ya miaka nane hufanywa na ndugu wa karibu,
Kuna madhara makubwa ya kutokuwa karibu na watoto, kuna kisa kimoja watoto wa mama mmoja baba mmoja kaka yao alikuwa anawaingilia kinyume na maumbile wadogo zake wawili chini ya miaka 10 bila wazazi wao kujua kutokana na ubize wa kuondoka asubuhi na kurudi usiku nyumbani" alisema Mwandila.
Program Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto iliyozinduliwa mwaka 2021, inayotekelezwa kwa miaka mitano yaani (2021/2022-2025/2026 inasisitiza wazazi ,walezi na jamii kuhakikisha wanawekeza kwa watoto kuanzia miaka 0-mpaka miaka 8 katika afua muhimu za lishe, afya , elimu, ulinzi na usalama pamoja na uchangamshi wa awali ili kufikia kikamilifu hatua za ukuaji.
MATOKEO ya Tanzania Vs Guinea Leo Tarehe 10 September 2024
MATOKEO ya Tanzania Vs Guinea Leo Tarehe 10 September 2024
Guinea inacheza na Tanzania katika Raundi ya Awali ya Kombe la Mataifa ya Afrika mnamo Septemba 10. Mechi hiyo itaanza saa 19:00 kwa saa za kwenu.
Timu ya taifa ya kandanda ya Guinea na timu ya taifa ya kandanda ya Tanzania zinakutana tena miaka 4 baada ya mchezo wa Hatua ya Makundi uliomalizika kwa sare ya 2-2. Timu ya taifa ya kandanda ya Guinea iko katika hali mbaya inapokaribia mpambano huu baada ya kushindwa kutoka kwa DR Congo na Msumbiji. Kocha na wachezaji huenda wakaweka juhudi za ziada kwenye safu ya ulinzi kwani wamekuwa wakiruhusu mabao kwa mechi 4 mfululizo sasa.
Timu ya taifa ya soka ya Tanzania inashuka dimbani baada ya kucheza sare ya bila kufungana dhidi ya Etheopia Jumatano iliyopita na kuendeleza mfululizo wa kutopoteza hadi mechi 5. Inaonekana hawapaswi kuwa na matatizo mengi katika kujilinda kuwa na laha 5 mfululizo safi.
Udaku Special inaangazia Guinea dhidi ya Tanzania kwa wakati halisi, ikitoa mtiririko wa moja kwa moja na matokeo ya moja kwa moja ya mechi, orodha ya timu, takwimu kamili za mechi, maoni ya mechi ya moja kwa moja na muhtasari wa video rasmi. Tunashughulikia mechi zote za awamu ya Awali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wakati halisi na kutoa utiririshaji wa moja kwa moja inapowezekana.
MATOKEO TAIFA STARS Vs GUINEA
19:00 : TANZANIA 0: 0 GUINEA
Source
WANANCHI TUMULI NA IGUGUNO WAHAMASISHWA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

"Tujitokeze kwa wingi kuwania nafasi za Uongozi lakini pia tujitokeze kwa wingi kwenye mikutano ya siasa ili tuweze kusikiliza sera za viongozi wetu tunaotaka kuwachagua, na itakapofika Novemba 27, 2024 ukapige kura kumchagua kiongozi unayemtaka." DED Asia Messos
Vile vile amesisitiza juu ya kuchagua viongozi makini wazalendo wenye kiu ya kuleta maendeleo kwa wananchi na si wabinafsi, "Lakini tunapoenda kuchagua viongozi wetu, tusichague ili mradi tumechagua, chagueni viongzi wenye shahuku ya kuleta maendeleo" DED Asia Messos
Akizungumzia kuhusu zoezi la kuandikisha wapiga kura, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bi. Asia Messos amesema mchakato wa kuandika wapiga Kura kwenye Daftari la Orodha ya Wapiga Kura utaanza Oktoba 11-21,2024 na kuwataka wananchi wajitokeze kujiandikisha katika daftari hilo.
"Ili uweze kupiga kura unapaswa uwe umejiandikisha kwenye Daftari la Orodha ya Wapiga Kura, mchakato huu utaanza Tarehe 11-20, Oktoba 2024, itakapofika hii tarehe twendeni kwa pamoja tukajiandikishe tupate nafasi ya kuchagua viongozi wetu tunaowataka" Bi. Asia Messos
Aidha Bi. Asia Messos amewakumbusha wakazi wa kata hizo juu ya umuhimu wa kulinda miundombinu ya serikali, kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa kutoa taarifa kwenye mamlaka husika, kuhakikisha wanashiriki katika shughuli za maendeleo pamoja na kuchangia chakula shuleni.
Edo Kumwembe 'Huu Ndio Unafiki wa Watanzania Kwa Bwana Samatta'
Source
Sunday, September 8, 2024
Polisi Wafunguka Kuhusu Aliyetekwa Tegeta na Kukutwa Ameuawa Ununio....
SIMANZI: Kibao Akutwa Amefariki Ununio Baada ya Kutekwa Maeneo ya Tegeta
Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe, Viongozi na Wafuasi wengine wa Chama hicho pamoja na Wananchi wengine wamefika Hospitali ya Mkoa wa Kinondoni, Mwananyamala leo September 08,2024 kufuatia mwili wa aliyekuwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)Taifa na Msaidizi wa Katibu Mkuu, Ali Mohamed Kibao ambaye aliliripotiwa kutekwa juzi , kukutwa Hospitalini katika chumba cha kuhifadhia maiti ukiwa umeharibika.
Taarifa iliyotolewa leo Sept 8, 2024 kupitia ukurasa wa mtandao wa X(zamani Twitter) na Meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob imesema "Mwili wa Kibano ulikutwa umetupwa jana alfajiri maeneo ya UNUNIO (jirani na viwanja vya NSSF) ukiwa na majereha makubwa sehemu za usoni kiasi Ndugu zake walipata tabu kuutambua kirahisi, kwa mujibu wa Wenyeji wa Ununio ambao ni walima mchicha, wanasema jana asubuhi walitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi baada ya kuona mwili wa Mtu mzima, mweupe mwenye asili ya kiarabu ambaye baadaye Jana jioni ndugu waliutambua kuwa ni mwili Ali Mohammed Kibao ukiwa na majeraha"
Itakumbukwa jana September 7, 2024 Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika aliongea na Waandishi wa Habari na kusema Kibano alikamatwa na Watu wanaodhaniwa kuwa ni Askari Polisi eneo la Tegeta baada ya gari mbili za Jeshi la Polisi kuzuia basi la Tashrif lenye namba T 343 EES alilokuwa amepanda kutoka Dar kwenda Tanga kisha Watu wenye silaha ikiwemo bunduki wakaondoka nae ambapo baadaye Polisi kupitia kwa Msemaji wake David Misime walisema wameiona taarifa hiyo na wameanza uchunguzi.
Kabla ya umauti wake Ali Kibao aliwahi kuwa Afisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akastaafu na kujiunga na CCM, baadaye akachaguliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Tanga wakati wa Rais Mstaafu Kikwete na baadaye alijiunga CHADEMA.
Babati mji waahidi kuifanyia kazi ripoti ya Marafiki wa Elimu kuhusu Elimu jumuishi.
Na John Walter -Babati
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...