Friday, October 3, 2025

TAMASHA LA SIKU YA WANA 'STAND UNITED" NI KESHO JUMAMOSI CCM KAMBARAGE



Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro ambaye ni mlezi wa Timu ya Stand United akizungumza na waandishi wa habari.

Na Marco Maduhu,SHINYANGA


WANANCHI na mashabiki wa soka mkoani Shinyanga wametakiwa kujitokeza kwa wingi kesho, kushuhudia Tamasha la Siku ya Wana, litakalofanyika Uwanja wa CCM Kambarage, ambapo kutakuwa na utambulisho wa wachezaji wapya wa Timu ya Stand United watakaoshiriki Ligi ya Championship msimu huu.


Wito huo umetolewa leo Oktoba 3,2025 na Mlezi wa Timu ya Stand United Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro,wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea kwenye Tamasha hilo hapo kesho,ambalo litafanyika katika Uwanja wa CCM Kambarage.
"Natoa wito kwa wananchi wa Shinyanga na wapenzi wote wa soko wajitokeze kwa wingi hapo kesho kwenye Tamasha la siku ya wana ili kutoa Motisha kwa Timu yao ya Stand United, na kuishuhudia ikishuka dimbani dhidi ya Timu ya Pamba Jijiji katika mchezo wao wa kirafiki,"amesema Mtatiro.


Aidha,amesema katika msimu uliopita wa Ligi ya Champioship,ambapo Timu hiyo ili cheza Playoff ili kufuzu kushiriki Ligi kuu, kwamba wamejifunza mengi na msimu huu wa Championship timu ambazo watakutananazo ni kichapo tu sababu wamejipanga vizuri.
Msemaji wa Timu ya Stand United Ramadhan Zorro,amesema wamefanya usajiri mzuri na wachezaji wao wana viwango bora kabisa na kwamba kwa uwezo walio nao lazima watarejea kucheza Ligi kuu.


Amesema katika mchezo wao kesho dhidi ya Pamba Jijiji kwenye Tamasha hilo, wataonyesha uwezo wa wachezaji wao huku akiionya Pamba ijiandae kubeba mzigo wa magoli sababu wapo kamili.
Naye Msemaji wa Timu ya Pamba Jijiji Moses William,wamesema Timu ya Stand United ni nzuri na kwamba wamejipanga vyema kupata ushindi kwenye Tamasha hilo na hawatakuwa na mzaha.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tamasha hilo Chripin Kakwaya,amesema maandalizi ya Tamasha hilo yanaendelea vizuri, na kwamba wakati wa Tamasha hilo kutakuwa na burudani mbalimbali ambapo wataanza na Jonging kilomita 5,Mbio za Baiskeli na Burudani kutoka wa Wasanii.
Amesema, pia kutakuwa na michezo ya utangulizi kati ya timu ya Bajaji na Bodaboda, Soko Kuu na Soko la Majengo pamoja na Dabi ya Upongoji FC na Ibinzamata, na baada ya hapo Timu ya Stand United itashuka dimbani dhidi ya Pamba Jiji.


Ameongeza katika Tamasha hilo kutakuwa na viingilio ambapo mzunguko sh.3,000,VIP Sh.5000 na VVIP sh.10,000.


TAZAMA PICHA👇👇


Mwenyekiti wa Tamasha la siku ya wana Chripin Kakwaya akizungumza na waandishi wa habari.
Msemaji wa Timu ya Stand United Ramadhan Zorro akizungumza na waandishi wa habari.
Msemaji wa Timu ya Pamba Jijiji Moses William akizungumzia mchezo wao wa kesho dhidi ya Stand United.
Msemaji wa Timu ya Pamba Jijiji Moses William(kushoto)wakipongezana na Msemaji wa Timu ya Stand United Ramadhan Zorro.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...