Tuesday, April 8, 2025
Mhagama aongoza msafara wa Tanzania mkutano wa 150 mabunge ya duniani Uzbekistan
Mbunge wa Jimbo la Madaba Joseph Kizito Mhagama, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wabunge Wawakilishi wa umoja wa Mabunge Duniani kutoka Tanzania, ameongoza msafara wa Wabunge wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano wa 150 wa Mabunge Duniani (IPU) unaoendelea mjini Kashkenti, Uzbekistan, kuanzia Aprili 5 mpaka 9, 2025.
Katika mkutano huu, Mhagama ameonyesha juhudi za Bunge la Tanzania katika kuisimamia serikali na kuhakikisha kwamba inatekeleza majukumu yake kikamilifu, hasa katika nyanja za maendeleo na haki za binadamu.
Mkutano huo unazungumzia nafasi ya Mabunge katika kupigania maendeleo na haki za jamii (Social Development and Justice), ambapo Bunge la Tanzania limekuwa na nafasi muhimu katika kuhamasisha na kutunga sheria zinazolenga kuboresha hali ya maisha ya wananchi.
Mhagama ameelezea hatua muhimu ambazo Tanzania imechukua katika kuimarisha maendeleo ya kijamii na haki za binadamu, akisisitiza umuhimu wa Mabunge duniani kushirikiana ili kufikia malengo ya pamoja ya maendeleo endelevu.
Huu ni mkutano wa kihistoria ambao umeipa Tanzania fursa ya kuonyesha mchango wake katika masuala haya ya kimsingi, huku ikiendelea kujenga mifumo bora ya utawala inayozingatia haki na maendeleo ya wananchi wake.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...


