Tuesday, April 8, 2025
Mhagama aongoza msafara wa Tanzania mkutano wa 150 mabunge ya duniani Uzbekistan
Mbunge wa Jimbo la Madaba Joseph Kizito Mhagama, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wabunge Wawakilishi wa umoja wa Mabunge Duniani kutoka Tanzania, ameongoza msafara wa Wabunge wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano wa 150 wa Mabunge Duniani (IPU) unaoendelea mjini Kashkenti, Uzbekistan, kuanzia Aprili 5 mpaka 9, 2025.
Katika mkutano huu, Mhagama ameonyesha juhudi za Bunge la Tanzania katika kuisimamia serikali na kuhakikisha kwamba inatekeleza majukumu yake kikamilifu, hasa katika nyanja za maendeleo na haki za binadamu.
Mkutano huo unazungumzia nafasi ya Mabunge katika kupigania maendeleo na haki za jamii (Social Development and Justice), ambapo Bunge la Tanzania limekuwa na nafasi muhimu katika kuhamasisha na kutunga sheria zinazolenga kuboresha hali ya maisha ya wananchi.
Mhagama ameelezea hatua muhimu ambazo Tanzania imechukua katika kuimarisha maendeleo ya kijamii na haki za binadamu, akisisitiza umuhimu wa Mabunge duniani kushirikiana ili kufikia malengo ya pamoja ya maendeleo endelevu.
Huu ni mkutano wa kihistoria ambao umeipa Tanzania fursa ya kuonyesha mchango wake katika masuala haya ya kimsingi, huku ikiendelea kujenga mifumo bora ya utawala inayozingatia haki na maendeleo ya wananchi wake.
Source
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...


