Wednesday, September 25, 2024

MWANAMUZIKI LINAH AVURUGWA KUITWA BIBI KIZEE

MWANAMUZIKI LINAH AVURUGWA KUITWA BIBI KIZEE


Msanii wa Bongo Fleva, Esterina Sana maarufu kama Linah amewajia juu baadhi ya watu ambao wamekuwa wakimchamba mitandaoni kuwa amezeeka.


Kupitia Insta Story yake Linah ameandika; "Nashangazwa sana na watu wanavyoshambulia wenzao kuhusu kuzeeka dah, tena mtu anacheka kabisa 'Umezeeka' swali ni kwamba kwani wenzetu nyinyi mpo palepale?umri hausogei au mlishushwa tu hamkuzaliwa".


"Yaani mtu baada kumshukuru Mungu unaishi miaka mingi unaanza kutia kasoro duh, nina furaha na miaka 34 yangu kikubwa pumzi jamani".

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...