Thursday, September 12, 2024
Airtel Africa Foundation yazindua ‘Airtel Africa Fellowship Program’ kuwawezesha wanafunzi wa IIT Madras Zanzibar
Airtel Africa Foundation imezindua programu maalum ya uanazouni iitwayo 'Airtel Africa Fellowship' itakayowanufaisha wanafunzi wa shahada ya kwanza ya IIT Madras Zanzibar ambayo ni kampasi ya kigeni ya kwanza kuwahi kuanzishwa na IIT.
Programu ya 'Airtel Africa Fellowship' inalenga kuwasaidia wanafunzi wanaotoka kwenye uchumi na jamii mbalimbali ambao wanastahiili kujiunga na shahada ya sayansi ya TEHAMA Pamoja na kujifunza maswala ya akili mnemba yanayotolewa na taasisi ya teknolojia ya Madras (IITM) visiwani Zanzibar. Kwa hatua ya awali Airtel imeanza na dola za kimarekani $500,000, programu hii itawanufaisha wanafunzi 10 wa shahada ya kwanza katika kipindi chote cha miaka minne ya masomo yao.
Programu ya 'Airtel Africa Fellowship' imeanza rasmi mwaka huu 2024 ikiwa na lengo kusaidia maendeleo ya Afrika ambapo Airtel Africa Foundation imedhamiria kuendeleza ujumuishwaji wa kifedha na kidijitali katika maeneo mbalimbali kwa kuzingatia zaidi sekta ya elimu na utunzaji wa mazingira.
Programu hii ya uanazuoni ni mpango wa kwanza kuwahi kutekelezwa ili kuboresha fursa za elimu kwa ajili ya wanafunzi wanaostahili, hususani wale wanaotoka kwenye hali duni, ambao wamejiunga na IITM Zanzibar.
Programu hii imeundwa kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi kutoka nchi 14 za Afrika ambazo ni Nigeria, Kenya, Malawi, Uganda, Zambia, Tanzania, Rwanda, DRC, Niger, Congo Brazzaville, Chad, Gabon, Madagascar na Seychelles.
Wanufaika wa udhamini huu watajulikana kama 'Airtel Africa Fellows' ambao watapokea asilimia 100 ya ada zao za chuo ambazo ni dola za kimarekani $12,000 kulingana na mchanganuo wa ada ya taasisi hiyo kwa ajili ya programu ya miaka minne. Pia watapatiwa dola za kimarekani $500 kwa ajili ya gharama za kujikimu ambazo zitatolewa kwa wanafunzi wanaostahili.
Mpango huu unalenga kubadilisha maisha na kuwaandaa viongozi wa baadae ambao watachangia katika ubunifu wa teknolojia na ukuaji wa kiuchumi barani Afrika.
Akizungumzia mpango huo wa uanazuoni, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Zanzibar, Mheshimiwa, Lela Mohamed Mussa alisema, "IITM Zanzibar imeandaa utaratibu bora wa elimu ya kiufundi katika ukanda huu. Kutoa elimu ya hali ya juu kwa wanafunzi nchini Tanzania na bara la Afrika kwa ujumla ambao wamefanya vizuri katika michakato ya usahili na mitihani, msaada kifedha ni kipaumbele muhimu kwetu. Tunashukuru kwa msaada huu kutoka Airtel Africa Foundation ambao utaboresha jitihada zetu binafsi kupitia mwelekeo huu."
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Airtel Africa Foundation, Dkt Olusegun Ogunsanya alisema, "Tunafuraha ya kushirikiana na IITM Madras Zanzibar kutoa fursa kwa vijana wa kiafrika waweze kupata elimu bora. Mpango huu unalenga kuchangia katika ukuaji wa bara la Afrika. Tunatarajia kuendelea kutengeneza fursa nyingi zaidi kwenye elimu pamoja na ujumuishi wa huduma za kifedha kidijitali na kulinda mazingira.
Naye Mkurugenzi wa IIT Madras, Prof Veezhinathan Kamakoti alisema, "IIT Madras imejidhatiti kwa kuanzisha kampasi yenye ubora duniani visiwani Zanzibar. Tunafarijika kuaona Airtel Africa Foundation imetuunga mkoni katika jitihada hizi. Tunatarajia kukaribisha awamu ya pili ya wanafunzi kujiunga na kampasi ya IITM Zanzibar mwaka huu. Tunaishukuru sana Airtel Africa Foundation kwa kutoa msaada wa kifedha kwa ajili ya hawa viongozi wa taifa la baadae."
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
