Tuesday, August 20, 2024

VIDEO: Tunataka 'afande' afikishwe mahakamani-TLS


Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kimelitaka Jeshi la Polisi kumfikisha mahakamani mtu aliyetambulika kwa jina la 'afande' ambaye anadaiwa kuwatuma vijana wanne waliohusika kumbaka na kumlawiti binti kisha video hizo kusambaa mitandaoni.

Akizungumza na vyombo vya Habari, rais wa TLS, Boniface Mwabukusi amesema mtu huyo aliye nyuma ya tukio hilo amehusika kwenye uhalifu huo hivyo afikishwe mahakamani mara moja, huku akieleza kuwa TLS itafuatilia kwa ukaribu shauri hilo ili binti huyo apate haki yake.

"Tunataka aliyesababisha kitendo kile kufanyika na yeye ni mkosaji, afikishwe mahakamani mara moja. TLS itaona namna bora ya kuweka wakili atakayekuwa akifuatilia ili kuona maendeleo ya shauri lile yatakavyokuwa yakiendelea na kuhakikisha kuwa haki za binti yule hazipotei," amesema Mwabukusi.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...