Thursday, August 15, 2024

UTEUZI: Rais Samia Ateuwa Mawaziri, Ahamisha Viongozi

 

UTEUZI: Rais Samia Ateuwa Mawaziri, Ahamisha Viongozi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi na uhamisho wa viongozi mbalimbali huku akimteuwa Prof. Palamagamba Kabudi kuwa Waziri wa Katiba na Sheria;


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, imeeleza kuwa William Lukuvi ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), huku Jenista Mhagama akiteuliwa kuwa Waziri wa Afya.


Kabla ya uteuzi huo, Mhagama alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) na Balozi Dkt. Pindi Chana yeye ameteuliwa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.


Kabla ya uteuzi huo, Chana alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria, na sasa anachukua nafasi ya Angellah Jasmine Kairuki ambaye ameteuliwa kuwa Mshauri wa Rais.


Viongozi wengine walioteuliwa na kuhamishwa vituo vya kazi ni kama inavyoonekana katika viambatanishi.

UTEUZI: Rais Samia Ateuwa Mawaziri, Ahamisha Viongozi






Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...