Sunday, August 4, 2024

APR ya Rwanda kuchuana na Simba kwenye siku yao leo.


Na John Walter -Babati 

Klabu ya Simba leo itachuana na wageni wao APR FC katika mchezo wa kirafiki ambao ni sehemu ya sherehe ya Simba Day.

Mchezo huu utapigwa kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, ukiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 88 tangu kuanzishwa kwa klabu hiyo yenye makazi yake Kariakoo, Ilala.

APR FC, mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Rwanda, walifika jijini Dar es Salaam asubuhi ya Ijumaa, Agosti 2, wakiwa na kikosi cha wachezaji 24. Kati ya hao, kuna wachezaji 10 wapya waliojiunga na timu msimu huu, akiwemo Lamine Bah kutoka Mali, pamoja na Wanaigeria Johnson na Odibo.

Baadhi ya wachezaji wa APR FC waliokosa safari ni Nshimirimana Ismael Pichou, Apam Bemol ambaye alipoteza nafasi yake katika kikosi cha kwanza, na Kwitonda Alain Bacca ambaye hajaonyesha uwezo wa kumvutia kocha.

Aidha, kipa wa tatu Ivan Ruhamyankiko naye hakusafiri. APR FC iliwahi kucheza Tanzania Julai 21, 2024, ambapo walipoteza mchezo wa fainali ya Kombe la Kagame CECAFA dhidi ya Red Arrows.

Hii itakuwa fursa nyingine kwa APR FC kujipima nguvu dhidi ya timu kubwa ya Simba kabla ya kuelekea mechi yao ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Azam FC itakayofanyika Agosti 18 kwenye uwanja wa Compex Chamazi.

Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...