Thursday, July 25, 2024

Msichana Aliyemkata Uume Mchumba Wake Akamatwa Mpakani Tanzania



Polisi katika Wilaya ya Kyotera Mkoa wa Kati nchini Uganda wanamshikilia, Harriet Ampayire (23) kwa tuhuma za kukata sehemu za siri za mchumba wake na kusababisha kifo chake.

Harriet inadaiwa alifanya uhalifu huo kwa aliyekuwa mpenzi wake Reagan Karamagi, Jumapili Julai 21, 2024 kisha kutoroka.

Msemaji wa Polisi Kanda ya Kusini, Twaha Kasirye amethibitisha kukamatwa kwa Harriet na kueleza kuwa atakabiliwa na mashtaka ya mauaji baada ya upelelezi kukamilika.

"Mtuhumiwa alitaka kukimbia kwa kuvuka mpaka wa Mutukula ili kuingia Tanzania. Hata lakini tulifanikiwa kumkamata Jumanne," amesema Kamanda Kasirye.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Mutukula, David Mujaasi amesema mpaka huo unatumika na wahalifu wengi kutoroka nchini humo baada ya kufanya matukio ya uhalifu.

"Tunaiomba Serikali ituchukulie hatua kuimarisha ulinzi kwa sababu tuko katika eneo ambalo wahalifu wanalitumia kupita," amesema.

Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...