Saturday, July 27, 2024

Kisa Yanga Fei Toto Ashindwa Kusajiliwa Kaizer Chiefs na Mamelodi



KISA YANGA FEI TOTO ashindwa kununuliwa MAMELOD na KAIZER CHIEFS

Kiungo wa Azam Feisal Salum Abdallah (Fei Toto) amejikuta akipitwa na bahati za kucheza kwenye timu kubwa za Afrika kwasababu ya Kigezo kilichowekwa na Yanga kwenye mkataba wake wa kwenda Azam

Klabu ya Yanga na Azam walikubaliana kwamba Endapo Fei toto atauzwa na Azam kwenda timu yoyote basi Azam wanatakiwa wailipe YANGA Shilingi Billion 1 za Kitanzania, kitu ambacho kimefanya iwe kazi ngumu kwa Feitoto kuuzika kwasababu dau lake linaanzia Billion 1

Klabu mbalimbali zikiwemo MAMELOD SUNDOWNS na KAIZER CHIEFS zilituma maombi ya kumtaka Mzanzibari huyo lakini bei waliyopewa wenyewe wakashangaa😂😂😂

Ikumbukwe sio kwamba Azam wanataja bei kubwa kwa kupenda ila ni mkataba ndo unawafunga mpaka pale miaka 3 itakapoisha

Je, miaka 3 ikishaisha bado fei atahitajika nje ya nchi???
.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...