Tuesday, June 8, 2021
Rais Samia kufanya ziara ya siku tatu Jijini Mwanza
Rais Samia Suluhu anatarajiwa kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu mkoani Mwanza, ambapo pamoja na mambo mengine atazindua na kuweka jiwe la msingi kwenye miradi ya maendeleo ya mabilioni iliyoko mkoani hapa.
Akizungumza jana juu ya ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Albert Chalamila alisema ziara hiyo itaanza rasmi Juni 13 hadi Juni 15 mwaka huu, ambapo Rais atawasili jijini hapo akitokea mjini Dodoma ambapo atapata fursa ya kufungua mtambo mkubwa wa kusafisha dhahabu
Alisema mtambo huo umejengwa katika Kiwanda cha Mwanza Precious Metal Refinery katika manispaa ya Ilemela kwa gharama ya kiasi Sh bilioni 10.4.
Sambamba na kiwanda hicho pia siku hiyo Rais atafungua jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Kanda ya Mwanza ambao ujenzi wake tayari umekamilika.
"Rais mara baada ya kuzindua jengo hilo la BOT, atapata fursa ya kuhutubia wananchi," alisema Chalamila na kuwataka wakazi wa jiji la Mwanza kujitokeza kwa wingi siku hiyo akisisitiza kuwa hii ndiyo ziara ya kwanza ya Rais mkoani Mwanza baada ya kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya sita kwa mujibu wa Katiba baada ya aliyekuwa Rais wa awamu ya tano John Magufuli kufariki dunia.
Chalamila aliongeza kuwa Juni 14 Rais atakwenda wilayani Misungwi ambapo atazindua mradi wa maji Misungwi uliogharimu kiasi cha Sh bilioni 13.7 na kuhutubia wananchi.
"Baadaye Mheshimiwa Rais atakwenda kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa(SGR) eneo la Fela wilayani Misungwi huo ukiwa ni ujenzi wa loti ya tano," alisema Chalamila na kumshukuru Rais Samia kutokana na kasi na dhamira aliyoionyesha kwenye mradi huo ambapo tayari serikali imeishatoa kiasi cha Sh bilioni 372 ikiwa ni malipo ya awali kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo.
Chalamila amefafanua kuwa Juni 15 mwaka huu, Rais Samia Suluhu Hassan atatembelea na kukagua ujenzi wa mradi wa daraja la JPM unaojengwa kwa gharama ya Sh bilioni 699 ili aweze kujionea maendeleo ya ujenzi wake.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
