Tuesday, June 8, 2021
Rais Samia kufanya ziara ya siku tatu Jijini Mwanza
Rais Samia Suluhu anatarajiwa kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu mkoani Mwanza, ambapo pamoja na mambo mengine atazindua na kuweka jiwe la msingi kwenye miradi ya maendeleo ya mabilioni iliyoko mkoani hapa.
Akizungumza jana juu ya ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Albert Chalamila alisema ziara hiyo itaanza rasmi Juni 13 hadi Juni 15 mwaka huu, ambapo Rais atawasili jijini hapo akitokea mjini Dodoma ambapo atapata fursa ya kufungua mtambo mkubwa wa kusafisha dhahabu
Alisema mtambo huo umejengwa katika Kiwanda cha Mwanza Precious Metal Refinery katika manispaa ya Ilemela kwa gharama ya kiasi Sh bilioni 10.4.
Sambamba na kiwanda hicho pia siku hiyo Rais atafungua jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Kanda ya Mwanza ambao ujenzi wake tayari umekamilika.
"Rais mara baada ya kuzindua jengo hilo la BOT, atapata fursa ya kuhutubia wananchi," alisema Chalamila na kuwataka wakazi wa jiji la Mwanza kujitokeza kwa wingi siku hiyo akisisitiza kuwa hii ndiyo ziara ya kwanza ya Rais mkoani Mwanza baada ya kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya sita kwa mujibu wa Katiba baada ya aliyekuwa Rais wa awamu ya tano John Magufuli kufariki dunia.
Chalamila aliongeza kuwa Juni 14 Rais atakwenda wilayani Misungwi ambapo atazindua mradi wa maji Misungwi uliogharimu kiasi cha Sh bilioni 13.7 na kuhutubia wananchi.
"Baadaye Mheshimiwa Rais atakwenda kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa(SGR) eneo la Fela wilayani Misungwi huo ukiwa ni ujenzi wa loti ya tano," alisema Chalamila na kumshukuru Rais Samia kutokana na kasi na dhamira aliyoionyesha kwenye mradi huo ambapo tayari serikali imeishatoa kiasi cha Sh bilioni 372 ikiwa ni malipo ya awali kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo.
Chalamila amefafanua kuwa Juni 15 mwaka huu, Rais Samia Suluhu Hassan atatembelea na kukagua ujenzi wa mradi wa daraja la JPM unaojengwa kwa gharama ya Sh bilioni 699 ili aweze kujionea maendeleo ya ujenzi wake.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
