Thursday, June 17, 2021
Kilo 88 za dawa za kulevya zatelekezwa Ndani ya Prado Jijini Dar es Salaam
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) imefanikiwa kukamata kilo 88.27 za dawa za kulevya aina ya Heroin na Methamphetamine zikiwa ndani ya gari aina ya Toyota Prado iliyokuwa imetelekezwa barabarani.
Akizungumza leo juni 17, 2021 jijini Dar es Salaam, Kamishina Jenerali wa DCEA Gerald Kusaya amesema dawa hizo zimekamatwa Juni 2 mwaka huu, saa saba usiku katika eneo la Kimara Korogwe kwa ushirikiano wa DCEA na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
"Baada ya upekuzi wa kisheria kufanyika ndani ya gari kulipatikana na mifuko mikubwa mitatu aina ya sandarusi (viroba), ndani yake ikiwa na pakti 12 za dawa za kulevya aina ya Heroine zenye uzito wa kilo 12.25 pamoja na kontena za plastiki 73 ndani yake kukiwa na dawa aina ya Methaphetamine zenye uzito wa kilo 76.02," amesema Kamishina Jenerali Kusaya.
Aidha, Kamishna huyo ameeleza kuwa upelelezi bado unaendelea ikiwemo kumgundua mwenye gari hilo na mtanadao wake kwani dereva wa gari hilo baada ya kugundua anafuatilia alitelekeza gari hilo na kukimbia.
Kamishina Kusaya ameendelea kuto onyo kwa wanaojihusisha na biashara hiyo haramu kuacha kwani vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na mamlaka hiyo vipo macho.
"Ama zao, ama zetu lakini watambue Mamlaka tuko kazi muda wote na lengo letu ni kukomesha kabisa biashara hi haramu. Tunaomba wananchi waendelee kutoa taarifa ili kwa pamoja tushirikiane kukomesha dawa hizo," amesema Kamishna Kusaya.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
