Friday, May 28, 2021
Mwalimu akamatwa akijifanya Usalama wa Taifa ili atapeli
SALVATORY NTANDU
Jeshi la polisi mkoa wa shinyanga linawashikilia watuhumiwa watatu Dismond Zakaria mwalimu (33) Feisal Husein mtaalamu wa teknolojia ya mawasiliano (27) na Juma Almasi (35)mfanyabiashara kwa tuhuma ya kupatikana na nyaraka za serikali za kughushi kwa lengo la kufanya utapeli kwa wananchi.
Akizungumza na waandishi wa habari wilayani Kahama kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga (ACP) Debora Magiligimba amesema kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa mei 26 mwaka huu katika mtaa wa namanga wilayani humo katika msako maalumu wa kupambana na wahalifu.
Alisema kuwa baada ya kukamatwa walipatikana na nyaraka mbalimbali za serikali ikiwemo kitambulisho cha Idara ya usalama wa taifa,vitambulisho viwili vya jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) mhuri mmoja na barua mbalimbali zenye nembo ya jeshi la hilo.
"Watuhumiwa hawa hutumia magari mawili kufanya utapeli katika maeneo mbalimbali ya Tanzania yenye namba za usajili T 677 BMA Toyota Carina na T 110 DSX Toyota Rumion kwa kujiwasilisha kwa wafanyabiashara hususani watoa huduma za kifedha kuwa wao ni maafisa wa umma na wakifanikisha azima yao hutoroka,"alisema Magilimba.
Kamanda Magiligimba amesema kuwa watuhumiwa hao wanatumia vitambulisho vya Jeshi la wananchi viwili vyenye cheo cha Kanali na kimoja cha idara ya usalama wa taifa,pamoja na sare kwa lengo la kuwahadaa wananchi ili kujipatia fedha kwa njia isiyo halali huku wakijua wazi kuwa suala hilo ni kinyume cha sheria.
"Tumewakamata wakiwa na karatasi bandia zinazotumika kutapelia watoa huduma za za fedha,walikuwa wanatumia mbinu ya kuacha mabegi yao yenye karatasi hizo bandia katika ofisi hizo na kisha hurudi jioni na kuwaaminisha kuwa ni fedha halali,jambo ambalo halina ukweli wowote,"alisema Magiligimba.
Amefafanua kuwa mbinu nyingine inayotumiwa na watuhumiwa hao ni pamoja na kuwatongoza na kuwanywesha pombe wanawake na kuwaibia vitu vya thamani kama vile simu na fedha pamoja na kuwaahidi kuwapatia kazi kwa idara ya usalama wa taifa na jeshi la wananchi wa Tanzania.
"Bado tunaendelea kuwahoji na upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili na kuwaomba wananchi kuendelea kutoa taarifa pindi wanapowatilia shaka watu wanamna hiyo ambao hutumia vibaya nyaraka za serikali kujipatia kipato kwa njia isiyo halali,"amesema Magiligimba.
Mwisho
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
