Tuesday, May 18, 2021
Marekani Yaahidi Kuendeleza Ushirikiano Na Zanzibar Katika Kuimarisha Afya Za Wananchi Wake
Na Ramadhani Ali – Maelezo
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Donald Wright ameahidi Serikali ya nchi yake itaendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha afya za wananchi.
Ameeleza kuridhishwa na hatua kubwa iliyofikiwa katika mapambano dhidi ya maradhi ya Maleria na kusema kuwa Marekani itaendeleza mkakati utakaohakikisha maradhi hayo yanamalizika kabisa.
Balozi Donald ameeleza hayo alipofanya mazungumzo na Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui Ofisini kwake Mnazimmoja.
Balozi wa Marekani amemueleza Waziri wa Afya kuwa Serikali ya nchi yake imetenga fedha maalumu kwa ajili ya kupambana na maradhi ya Ukimwi nchini Tanzania.
Ameahidi kuwa nchi hiyo ipo tayari kusaidia masuala ya chanjo ya Covid 19 ili Zanzibar iendelee kuwa salama na maradhi hayo ambayo yamekuwa tatizo kubwa katika nchi nyingi duniani.
Aidha Balozi Donald ameeleza suala la Wafanyabiashara wa Marekani kuja kuwekeza vitega uchumi Zanzibar ili kuwapatia vijana wengi ajira na kuimarisha uchumi wan chi.
Amesema vijana ndio nguvu kazi ya nchi na iwapo watapatiwa ajira za uhakika wataweza kusaidia maendeleo ya nchi yao kwa kiwango kikubwa na kuipunguzia Serikali gharama zisizokuwa na ulazima.
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui amemueleza Balozi Donald kuwa maradhi ya Maleria yapo kwa asilimia moja hivi sasa na Wizara ya Afya huchukuwa hatua za dharura sehemu ambayo atapatikana mgonjwa wa maradhi hayo.
Akizungumzia maradhi ya Covid 19 Waziri Mazurui amesema kwa kipindi cha mwezi mmoja sasa Zanzibar hajapatikana mgonjwa wa maradhi hayo na tahadhari kubwa inaendelea kuchukuliwa kwa wenyeji na wageni wanaoingia nchini.
Amesema Zanzibar haijaweka vizuizi kwa watu kuingia na kutoka lakini milango mikuu yote ya kuingilia kumewekwa mashine maalumu za kufanyia uchunguzi ili kuhakikisha maradhi hayo hayaingia nchini.
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela amelishauri Kanisa la Kiinjili la Kilutheri ...
