Tuesday, May 18, 2021
Marekani Yaahidi Kuendeleza Ushirikiano Na Zanzibar Katika Kuimarisha Afya Za Wananchi Wake
Na Ramadhani Ali – Maelezo
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Donald Wright ameahidi Serikali ya nchi yake itaendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha afya za wananchi.
Ameeleza kuridhishwa na hatua kubwa iliyofikiwa katika mapambano dhidi ya maradhi ya Maleria na kusema kuwa Marekani itaendeleza mkakati utakaohakikisha maradhi hayo yanamalizika kabisa.
Balozi Donald ameeleza hayo alipofanya mazungumzo na Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui Ofisini kwake Mnazimmoja.
Balozi wa Marekani amemueleza Waziri wa Afya kuwa Serikali ya nchi yake imetenga fedha maalumu kwa ajili ya kupambana na maradhi ya Ukimwi nchini Tanzania.
Ameahidi kuwa nchi hiyo ipo tayari kusaidia masuala ya chanjo ya Covid 19 ili Zanzibar iendelee kuwa salama na maradhi hayo ambayo yamekuwa tatizo kubwa katika nchi nyingi duniani.
Aidha Balozi Donald ameeleza suala la Wafanyabiashara wa Marekani kuja kuwekeza vitega uchumi Zanzibar ili kuwapatia vijana wengi ajira na kuimarisha uchumi wan chi.
Amesema vijana ndio nguvu kazi ya nchi na iwapo watapatiwa ajira za uhakika wataweza kusaidia maendeleo ya nchi yao kwa kiwango kikubwa na kuipunguzia Serikali gharama zisizokuwa na ulazima.
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui amemueleza Balozi Donald kuwa maradhi ya Maleria yapo kwa asilimia moja hivi sasa na Wizara ya Afya huchukuwa hatua za dharura sehemu ambayo atapatikana mgonjwa wa maradhi hayo.
Akizungumzia maradhi ya Covid 19 Waziri Mazurui amesema kwa kipindi cha mwezi mmoja sasa Zanzibar hajapatikana mgonjwa wa maradhi hayo na tahadhari kubwa inaendelea kuchukuliwa kwa wenyeji na wageni wanaoingia nchini.
Amesema Zanzibar haijaweka vizuizi kwa watu kuingia na kutoka lakini milango mikuu yote ya kuingilia kumewekwa mashine maalumu za kufanyia uchunguzi ili kuhakikisha maradhi hayo hayaingia nchini.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
