Friday, March 26, 2021

Mke wa Tatu wa Mfalme Zwelithini Achaguliwa Kuwa Kiongozi wa Wazulu




Familia ya Kifalme ya Zulu nchini Afrika Kusini imemteua Mke wa tatu wa Mfalme Goodwill Zwelithini kushikilia nafasi ya Uongozi hadi pale Mfalme mpya atakapotawazwa.

 

 

Malkia Mantfombi Dlamini Zulu ameshikilia wadhifa wa Kimalkia tangu alipoolewa na Mfalme mwaka 1977. Uteuzi wake umeibua mjadala kwamba mmoja wa wanawe atakuwa Mfalme wa Wazulu.

 

 

Mfalme Zwelithini (72) alikuwa akiugua maradhi ya Kisukari na alifariki hospitalini kutokana na changamoto za kiafya zilizochochewa na Ugonjwa wa Corona tarehe 12 mwezi Machi. Alikuwa Mfalme kwa karibu miaka 50.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...