Sunday, January 31, 2021
Wakamatwa Kwa Madai Ya Wizi Wa Fedha Kwa Njia Ya Simu
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Ialla jijini Dar es Salaam linawashikilia watu 10 kwa tuhuma za wizi wa mtandaoni na utapeli.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa Ilala, Janeth Magomi imeeleza kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa katika tarehe tofauti ya mwezi Januari mwaka huu katika maeneo tofauti ya Jiji la Dar es Salaam na wilayani Mkuranga mkoani Pwani.
Aidha, Mgomi ameeleza kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) baada ya wananchi kadhaa kutapeliwa fedha zao. Wananchi hao walitoa taarifa kwa jeshi hilo ndipo ukafanyika msako pamoja na kuweka mtego wa kubaini mtandao wa watuhumiwa hao.
Kufuatia tukio hilo Jeshi la Polisi Mkoa wa Ilala limewatahadhariasha watumiaji wa huduma za mitandao kuwa makini na watu ambao mara nyingi wanajifanya ni watoa huduma za mitandao husika na kuwalaghai wananchi ili kuwaibia.
Miongoni mwa watuhumiwa waliotiwa mbaroni ni pamoja na Baraka Makwaya, Fatuma Ayoub, Teddy Njauz, Modesta Njauz pamoja na Gift Makwaya.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...