Tuesday, January 12, 2021
Utawala wa Donald Trump Wairudisha Cuba katika nchi zinazofadhili ugaidi
Utawala wa Rais Donald Trump umeirudisha Cuba katika orodha ya 'nchi zinazofadhili ugaidi' na kuiwekea vikwazo vipya vinavyoweza kukwamisha ahadi ya Biden kufufua uhusiano na serikali hiyo ya kikomunisti.
Waziri wa Mambi ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo, ametangaza hatua hiyo jana Jumatatu akitaja ushirikiano kati ya Cuba na waasi wa Colombia.
Aidha sababu nyingine ni ushirikiano wa Cuba na serikali ya siasa za mrengo wa kati ya Venezuela pamoja na hatua ya Cuba kuwakaribisha wakimbizi wa Marekani kuwa miongoni mwa sababu zilizowafanya kuchukua hatua hiyo.
Suala la kuitangaza Cuba kuwa taifa linalofadhili ugaidi limejadiliwa kwa miaka mingi na ni miongoni mwa hatua kadhaa za mwisho za sera ya nchi za nje ambazo utawala wa Trump unafanya kabla ya Biden kuchukua urais Januari 20.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
