Tuesday, January 12, 2021
Utawala wa Donald Trump Wairudisha Cuba katika nchi zinazofadhili ugaidi
Utawala wa Rais Donald Trump umeirudisha Cuba katika orodha ya 'nchi zinazofadhili ugaidi' na kuiwekea vikwazo vipya vinavyoweza kukwamisha ahadi ya Biden kufufua uhusiano na serikali hiyo ya kikomunisti.
Waziri wa Mambi ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo, ametangaza hatua hiyo jana Jumatatu akitaja ushirikiano kati ya Cuba na waasi wa Colombia.
Aidha sababu nyingine ni ushirikiano wa Cuba na serikali ya siasa za mrengo wa kati ya Venezuela pamoja na hatua ya Cuba kuwakaribisha wakimbizi wa Marekani kuwa miongoni mwa sababu zilizowafanya kuchukua hatua hiyo.
Suala la kuitangaza Cuba kuwa taifa linalofadhili ugaidi limejadiliwa kwa miaka mingi na ni miongoni mwa hatua kadhaa za mwisho za sera ya nchi za nje ambazo utawala wa Trump unafanya kabla ya Biden kuchukua urais Januari 20.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
