Tuesday, January 19, 2021
Taifa Stars kuanza na Zambia leo michuano ya CHAN
Kuelekea kwenye mchezo huo, kocha wa Taifa Stars, Mrundi Etienne Ndayiragije amesema "maandalizi yameenda vizuri, wachezaji wapo sawa. Kuhusu korona wamechekiwa wote wako sawa, tuko vizuri. Tunaendeelea kujiandaa kwenye vile ambavyo tunaamini vitakuwa vya msaada kwetu".
Kuhusu nafasi ya Stars kwenye mchezo huo, Ndayiragije amesema " morali na hali ya kujiamini kuko juu kwenye kambi, wachezaji wapo tayari kwa mchezo, nimewaambia tutatcheza ili tushinde maana najua ushindi utainua ari kwenye kikosi na kupelekea tufanye vizuri kwenye michezo inayofuata".
Etienne amesema ari imeongezeka baada ya kocha msaidizi Selemani Matola kujiunga na kikosi hicho baada ya kumaliza majukumu ya kuiongoza kikosi cha Simba kwenye michuano ya Mapinduzi viswani Zanzibar na Erasto Nyoni akijiunga na timu baada ya kumaliza matatizo ya kifamilia.
Ushiriki wa Taifa Stars kwenye michuano ya CHAN umekuja baada ya miaka takribani 11 tokea ushiriki wao mwaka 2009 michuano hiyo ulipoanzishwa na ndiyo msimu ambapo Zambia walishiriki kwa mara ya kwanza na kushika nafasi ya 3 ikiwa ndiyo ya juu zaidi kwa upande wao kwenye CHAN.
Huu utakuwa mchezo wa 18 wawili hao kukutana, kwenye michezo 8 ya mwisho ambayo Stars imekutana na Zambia kwenye michuano tofauti kukiwa na mchanganyiko wa wachezaji wao wakigeni kwenye vikosi vyao, Zambia imeshinda mara 4, sare 3 wakati Stars imeshinda mara 1 pekee.
Ili Taifa Stars iweke hai matumaini ya kufuzu hatua inayofuata ya robo fainali, inahitaji ipate ushindi michezo yote mitatu ya makundi watakayocheza au kuwa na matokeo yatakayomfany awe na alama nyingi kuliko wote kwenye kundi D au alama nyingi zitakazomfanya ashike wapili kwenye kundi.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
