Sunday, January 3, 2021

Apiga piano kwa Saa 18, anataka kuvunja rekodi ya Guinness



Mpiga piano maarufu nchini China Liu Ji, alipiga piano kwa saa 18 mfululizo kuanzia saa moja asubuhi hadi siku ya pili saa saba usiku.


Mpiga piano huyu aliyekuwa mshindi mwenye umri mdogo zaidi katika Mashindano ya Kimataifa ya Piano ya Birmingham huko Uingereza.


Amesema anatumai wasikilizaji wanaweza kupata nguvu kutokana na muziki wake, pia alitaka kuonyesha heshimu yake kwa watu wanaofanya bidii katika kupambana na virusi vya Corona na kuchangia kwenye ujenzi wa taifa lake.


Hata hivyo lengo lake kubwa ni kuvunja rekodi wa 'Guinness World Records' kwa kupiga piano kwa saa 18 mfululizo.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...