Thursday, December 24, 2020
Washikiliwa kwa kumshambulia kwa ngumi, mateke dereva wa lori
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linawashikilia watu wanne akiwemo dereva wa basi la Kampuni ya Frester wakituhumiwa kwa kosa la kumshambulia dereva wa lori wakimtuhumu kwa kosa la kutaka kuwasababishia ajali.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Debora Magiligimba amewataja wanaoshikiliwa kuwa ni dereva wa basi la Kampuni ya Frester lenye namba za usajili T.915 CGU, Mwita Chacha mkazi wa wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga na abiria wake Joyce Charles.
Abiria wengine waliokamatwa ni Athumani Mussa na Christopher Rangati wote wakituhumiwa kwa kosa la kumshambulia kwa ngumi na mateke dereva wa lori, Emmanuel Msuya mkazi wa Moshi mkoani Kilimanjaro.
Kamanda Magiligimba amesema, tukio hilo lilitokea juzi katika eneo la Samuye wilayani Shinyanga na kwamba chanzo cha vurugu ni dereva wa basi la kampuni ya Frester kulibana ubavuni lori lililokuwa likisubiri kupimwa katika mzani wa kupimia magari uliopo Tinde wilayani Shinyanga.
Akifafanua amesema, lengo la dereva wa basi kulibana lori ni kutaka kupima haraka kabla ya lori ambapo hata hivyo dereva wa lori hakuruhusu basi hilo lipimwe kabla yake na yeye alipima na kuondoka kuendelea na safari bila ya kusababisha ajali yoyote eneo la mzani.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
