Tuesday, December 29, 2020
MAMIA WAMUAGA MNGEREZA DAR ES SALAAM
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa amesema Taifa limepata pigo kwa kuondokewa na Mtendaji wake mchapakazi, Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mngereza.
Waziri Bashungwa ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati wa shughuli ya kuaga mwili wa Mngereza katika viwanja vya Karimjee.
Amesema katika uhai wake Mngereza alisimamia Tasnia ya Sanaa na kuleta mabadiliko miongoni mwa Wasanii ambao wengi wao walifanya kazi zao kwa kuzingatia mila na desturi za Mtanzania.
Kwa mujibu wa Waziri Bashungwa, Serikali itaendeleza mambo mazuri aliyoyaacha Marehemu Mngereza, yaliyokuwa na lengo la kuleta mabadiliko kwa Wasanii na kazi zao.
Awali akimkaribisha Waziri Bashungwa, Msemaji Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt Hassan Abbasi amewataka Wasanii nchini na Watanzania wote kumuenzi kwa vitendo Marehemu Mngereza aliyejitolea na kuipenda kazi yake hadi umauti unamkuta.
Miongoni mwa Viongozi waliohudhuria shughuli hiyo ya kumuaga Marehemu Mngereza katika viwanja vya Karimjee ni Naibu Waziri Wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Abdallah Ulega, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge.
Mwili wa Mngereza unasafirishwa mchana huu kuelekea Suji, Same mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya.mazishi yatakayofanyika kesho.
Mngereza ameacha Mke na Watoto Watatu, ,Bwana ametoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe Amen.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
