Friday, November 27, 2020
Yafahamu mambo ambayo mwanamke anayahitaji katika mahusiano ya kimapenzi
1. Anataka mume anayemjali na kujali kila anachokitaka. Sio tu mahitaji ya kimwili, bali pia ayatambue mahitaji yake ya kisaikolojia, upendo na kujali hisia zake.
2. Anataka mume anayemlinda na kumfanya ahisi kuwa yuko salama wakati wowote, kiasi kwamba hana hofu ya chochote kwa sababu anajua kwamba mumewe atamlinda na kumkinga na maudhi.
3. Mume anayehisi kwamba ameshikamana naye na kuridhika naye.
4. Mume anayeshiriki naye katika maongezi matamu yenye hisia tamu. mume anayempa maneno laini, sio maongezi makavu yasiyokuwa na hisia za kimahaba.
5. Anataka mume anayembusu kila anapoagana naye au anapokutana naye. Mke anapenda jambo zuri linalofanywa mara kwa mara hata kama ni dogo, kuliko jambo kubwa linalofanywa kwa kuchelewa au kwa muda mrefu. Busu unalompa kila siku kabla ya kwenda kazini ni bora kwake kuliko "outing" unayompa baada ya miezi sita.
6. Anataka mume anayeyaona yanayofanywa na mkewe kwa ajili yake, hata kama ni madogo. "Attention" ya mume kwa mke ni jambo muhimu mno. Anataka attention yako kwenye mavazi, kwenye chakula na hata mabadiliko madogo anayoyafanya kwenye chumba chenu....sio unakuta kitanda kimebadilishwa mkao unaanza kuponda
7. Mke anataka mume anayemkubali vile alivyo na kuchunga sana usalama wa hisia zake. Usalama wa hisia za mwanamke ni muhimu mno kuliko hata usalama wa uchumi wake. Haitakuwa na maana kama unamnunulia mavazi mazuri, lakini ukawa unaziumiza hisia zake.
8.mke anataka mume mwenye imani asiyetereka wala kuyumbishwa kwa maneno ya dada zake hata wazazi wake anayeweza kujisimamia ,sio kuperekeshwa
Ili kujifunza zaidi namna ya kutunza na kuimarisha mahusiano yako Pia usisahau kusikiliza sauti ya Mungu na kutenga Muda wa kuomba zaidi.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
