Friday, November 27, 2020
Yafahamu mambo ambayo mwanamke anayahitaji katika mahusiano ya kimapenzi
1. Anataka mume anayemjali na kujali kila anachokitaka. Sio tu mahitaji ya kimwili, bali pia ayatambue mahitaji yake ya kisaikolojia, upendo na kujali hisia zake.
2. Anataka mume anayemlinda na kumfanya ahisi kuwa yuko salama wakati wowote, kiasi kwamba hana hofu ya chochote kwa sababu anajua kwamba mumewe atamlinda na kumkinga na maudhi.
3. Mume anayehisi kwamba ameshikamana naye na kuridhika naye.
4. Mume anayeshiriki naye katika maongezi matamu yenye hisia tamu. mume anayempa maneno laini, sio maongezi makavu yasiyokuwa na hisia za kimahaba.
5. Anataka mume anayembusu kila anapoagana naye au anapokutana naye. Mke anapenda jambo zuri linalofanywa mara kwa mara hata kama ni dogo, kuliko jambo kubwa linalofanywa kwa kuchelewa au kwa muda mrefu. Busu unalompa kila siku kabla ya kwenda kazini ni bora kwake kuliko "outing" unayompa baada ya miezi sita.
6. Anataka mume anayeyaona yanayofanywa na mkewe kwa ajili yake, hata kama ni madogo. "Attention" ya mume kwa mke ni jambo muhimu mno. Anataka attention yako kwenye mavazi, kwenye chakula na hata mabadiliko madogo anayoyafanya kwenye chumba chenu....sio unakuta kitanda kimebadilishwa mkao unaanza kuponda
7. Mke anataka mume anayemkubali vile alivyo na kuchunga sana usalama wa hisia zake. Usalama wa hisia za mwanamke ni muhimu mno kuliko hata usalama wa uchumi wake. Haitakuwa na maana kama unamnunulia mavazi mazuri, lakini ukawa unaziumiza hisia zake.
8.mke anataka mume mwenye imani asiyetereka wala kuyumbishwa kwa maneno ya dada zake hata wazazi wake anayeweza kujisimamia ,sio kuperekeshwa
Ili kujifunza zaidi namna ya kutunza na kuimarisha mahusiano yako Pia usisahau kusikiliza sauti ya Mungu na kutenga Muda wa kuomba zaidi.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...