Wednesday, November 25, 2020
Tanzania Yateuliwa Umoja Wa Mataifa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeteuliwa kuwa Mwenyekiti wa kamati ya hati za utambulisho ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN Credentials Committee) New York Marekani kwa mwaka 2020/2021.
Hii ni mara ya kwanza katika Historia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushika nafasi ya kuongoza kamati hiyo nyeti ya Umoja wa Mataifa ambapo uteuzi wake ulipendekezwa na Ofisi ya Rais wa Baraka Kuu la Umoja wa Mataifa na kuidhinishwa kwa kauli moja na wajumbe wote tisa wa Kamati hiyo.
Wajumbe hao ni Marekani,China,Urusi,Cameroon,Uruguay Iceland Papua Guinea na Trinidad na Tobagona na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akizungumza mara baada ya uteuzi huo Mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Prof. Kenedy Gaston amesema kuwa uteuzi huo ni muhimu sana na ni ishara ya namna Tanzania inakubalika katika uso wa Jumuiya ya Kimataifa kutokana na uongozi thabiti wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli halikadhalika sera zake za mambo ya nje.
Balozi Prof. Kenedy Gaston ameongeza kuwa kwa mara ya kwana tangu uteuzi huo Tanzania imeongoza kikao chake cha kwanza cha kamati hiyo Kikao kilichofanyika New York,Marekani.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
