Saturday, November 14, 2020
TAKUKURU na Mkurugenzi wa jiji Dar waokoa bil. 12 ujenzi wa stand ya Mbezi Luis
Mkurugenzi mkuu Takukuru, Brigedia John Mbungo amesema ofisi yake kwa kushirikiana na mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Zipora Liana wamedhibiti Sh12 bilioni ambazo zingelipwa kinyume na mipango katika mradi wa ujenzi wa stendi mpya ya mabasi mkoa wa Dar es Salaam.
Mbungo ameeleza hayo leo Jumamosi Novemba 14, 2020 katika mkutano wake na waandishi wa habari.
Amesema fedha hizo zilikuwa zinalipwa kwa makandarasi kama ziada kwa kazi ambayo haikufanyika.
"Udhibiti huu umefanikiwa kwa kuwa na wachunguzi na wataalamu wa ujenzi kutoka Takukuru waliokuwa wakifuatilia kazi hii kwa karibu," amesema.
Mbungo ametoa pongezi kwa Liana huku akitoa wito kwa wakurugenzi wengine kuendelea kushirikisha na taasisi hiyo kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kuhakikisha fedha za Serikali zinazotokana na kodi za wananchi zinatumika kulingana na malengo yaliyowekwa.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
