Monday, November 23, 2020
Hatua nne za kufikia malengo yako kwa uhakika mkubwa
Kila mtu katika maisha yake ana malengo maalumu ambayo anakuwa amejiwekea na anakuwa ana waza kwamba kwa namna yoyote ni lazima baada ya muda fulani malengo yake yatatimia.
Pia sina shaka na wewe, naamini umejifunza kwa sehemu namna au mbinu ambazo mtu anaweza akazitumia kuweza kufikia malengo yake. Lakini leo hii, si vibaya kama nitakung'ata sikio kukumbushia tena jinsi unavyoweza kufikia malengo yako kwa uhakika mkubwa.
Najua kila mtu ana njia zake na mbinu ambazo anazitumia kuweza kufikia malengo yoyote katika maisha. Leo hii, naomba nikuonyeshe mbinu ambazo zinatumiwa karibu na watu wote wenye mafanikio makubwa kufikia malengo yao kila wakati.
Andika malengo yako chini.
Yaweke malengo yako kwenye karatasii ili yawe rahisi kuyaona. Yawe ni malengo mahsusi ambayo utekelezaji wake unafikika na uwe tayari umejiwekea tarehe maalumu ya kuyafikia. Hio ndiyo sifa ya malengo unayotakiwa kuwa nayo.
Anza kuweka mipango.
Umesha andika malengo yako tayari. Hatua inayofuata ni kwa wewe sasa, kuweka mipango ya kufanya. Kumbuka unapofanya jambo unapata nguvu zaidi ya kuweza kulifanikisha kuliko ukitulia. Hivyo ni lazima mipango yako iwe hai na ya kiutekelezaji.
Lipa gharama.
Kubali kulipia kila gharama inayohitajika ili kufikia malengo yako. Gharama hizo zinaweza zikawa ni muda au nidhamu binafsi. Lakini gharama yoyote fanya kila ufanyalo hakikisha unailipa. Kama utakwepa kulipa gharama yoyote ile naomba nikwambie sahau mafanikio.
Yapitie malengo yako kila siku.
Hakuna namna ya nyingine ya kuwa mshindi zaidi ya wewe kukomaa kupitia malengo yako kila siku. Unapopitia malengo yako kila siku yanakupa nguvu na hamasa kubwa ya kuona ni jinsi gani yanawezekana na unaweza kuyafikia.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
