Tuesday, October 6, 2020
Aliyefungwa Jela Akiwa na Miaka 18 Aachiwa Akiwa na Miaka 100
Babu mwenye umri wa miaka 100 aliyekuwa anatumikia kifungo cha maisha jela kwa kosa la mauaji nchini Nigeria ameachiwa huru kwa msamaha wa Serikali.
Celestine Egbunuche ametumikia miaka 18 jela hadi wiki hii, baada ya kukutwa na hatia ya kupanga mauaji.
Baada ya kuachiwa huru, alikutana na familia yake nje ya gereza la Enugu ambalo lina ulinzi mkali zaidi. Mwanaye, Chisom Celestine alieleza jinsi alivyofurahi kumuona tena baba yake uraiani.
"Nilifurahi sana na ninamshukuru Mungu kwa siku hii. Mimi ni mtu mwenye furaha zaidi duniani sasa hivi," alisema.
Egbunuche ambaye hivi sasa anasumbuliwa na magonjwa kama kisukari na matatizo ya kuona, amewekwa chini ya uangalizi wa kimatibabu hospitalini.
Hata hivyo, mwanaye amesema kuwa hana uwezo wa kifedha wa kumsaidia baba yake kupata matibabu.
Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii imeendelea kufanya kampeni kutafuta namna ya kumsaidia.
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
