Thursday, July 2, 2020
Mwaandishi wa habari wa Muungwana Blog Zanzibar anyakua Tunzo 3 za utetezi wa watoto
Mwandishi wa Habari wa Muungwana Blog visiwani Zanzibar,Thabit Hamidu Madai amepata Tunzo Tatu ya Umahiri wa Uwandishi wa habari Mitandaoni kwa habari zinazohusu udhalilishaji na ukatili wa watoto visiwani Zanzibar.
Tunzo hizo zimetolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia haki za watoto Duniani (UNICEF) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Waandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA) na kukabidhiwa na Wazira wa Kazi,Uwezeshaji Wanawake,Wazee na Watoto Zanzibar, Moudline Cyrus Castico.
Hafla ya kukabidhi Tunzo ilifanyika katika Ukumbi wa Jumuiya walemavu Zanzibar uliopo weilesi Kikwajuni na kushirkisha Waandishi wa Habari, Wahariri wa vyombo vya Habari na wadau mbalimbali wa Habari kutoka ndani na nje ya Nchi.
Jumla ya Tunzo 9 zimetolewa ambazo ni Tunzo za Waandishi wa habari bora wa habari za watoto katika vipindi vya Redioni, Makala za magazeti, vipindi vya televisheni na Habari na makala za mitandaoni ambapo Thabit Madai alichukua nafasi kwanza,Nafasi ya Pili na Nafasi ya kwanza katika kundi la Mwandishi wa Habari za mitandao.
Akizungumza Mara baada ya kukabidhi Tunzo hizo, Wazira wa Kazi,Uwezeshaji Wanawake,Wazee na Watato Zanzibar,Moudline Cyrus Castico aliwataka waandishi wa Hbari kuongeza kasi katika kuandika habari zinazohusu changamoto za watoto visiwani humo ili Serikali na wadau mbalimbali kuweza kuzitatua.
"Waandishi wa Habari bado muna kazi kubwa sana ya kuandika hizi changamoto zinazowakabiliwa watoto visiwani Zanzibar ili zitatuliwe na watoto wetu waishi kwa amani, hivyo nawaomba zidisheni kasii hii kwa mashirikiano na Serikali" alisema Waziri Castico.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...