Thursday, July 2, 2020
Mwaandishi wa habari wa Muungwana Blog Zanzibar anyakua Tunzo 3 za utetezi wa watoto
Mwandishi wa Habari wa Muungwana Blog visiwani Zanzibar,Thabit Hamidu Madai amepata Tunzo Tatu ya Umahiri wa Uwandishi wa habari Mitandaoni kwa habari zinazohusu udhalilishaji na ukatili wa watoto visiwani Zanzibar.
Tunzo hizo zimetolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia haki za watoto Duniani (UNICEF) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Waandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA) na kukabidhiwa na Wazira wa Kazi,Uwezeshaji Wanawake,Wazee na Watoto Zanzibar, Moudline Cyrus Castico.
Hafla ya kukabidhi Tunzo ilifanyika katika Ukumbi wa Jumuiya walemavu Zanzibar uliopo weilesi Kikwajuni na kushirkisha Waandishi wa Habari, Wahariri wa vyombo vya Habari na wadau mbalimbali wa Habari kutoka ndani na nje ya Nchi.
Jumla ya Tunzo 9 zimetolewa ambazo ni Tunzo za Waandishi wa habari bora wa habari za watoto katika vipindi vya Redioni, Makala za magazeti, vipindi vya televisheni na Habari na makala za mitandaoni ambapo Thabit Madai alichukua nafasi kwanza,Nafasi ya Pili na Nafasi ya kwanza katika kundi la Mwandishi wa Habari za mitandao.
Akizungumza Mara baada ya kukabidhi Tunzo hizo, Wazira wa Kazi,Uwezeshaji Wanawake,Wazee na Watato Zanzibar,Moudline Cyrus Castico aliwataka waandishi wa Hbari kuongeza kasi katika kuandika habari zinazohusu changamoto za watoto visiwani humo ili Serikali na wadau mbalimbali kuweza kuzitatua.
"Waandishi wa Habari bado muna kazi kubwa sana ya kuandika hizi changamoto zinazowakabiliwa watoto visiwani Zanzibar ili zitatuliwe na watoto wetu waishi kwa amani, hivyo nawaomba zidisheni kasii hii kwa mashirikiano na Serikali" alisema Waziri Castico.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
